Friday 30 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Wenger awania Sentahafu
Baada ya kuwapoteza Masentahafu Sol Campbell, William Gallas, Mikael Silvestre na Sendoros, Arsenal imebakiwa na Masentahafu watatu tu na hilo limemfanya Bosi wa Arsenal Arsene Wenger kusaka Beki mmoja mpya.
Masentahafu waliobaki Arsenal ni Thomas Vermaelen, Mchezaji mpya Laurent Koscielny na Johan Djourou.
Wenger ametamka: “Tunasaka Mabeki wapya kwani tunahitaji tuwe na jumla ya Masentahafu watano. Inabidi tumpate mmoja kwa sababu tunao Wachezaji wanaoweza kucheza kwa dharura kama Sentahafu. Wapo tunaowalenga lakini kwa sasa siwezi kusema ni nani.”
Ufaransa Bingwa Ulaya Chini ya Miaka 19
Timu ya Taifa ya Ufaransa Chini ya Miaka 19 leo imewafunga Spain 2-1 na kutwaa Ubingwa wa Ulaya katika Fainali iliyochezwa Stade Michele d’Ornano Mjini Caen, Kaskazini ya Ufaransa.
Hadi mapumziko, Ufaransa ilikuwa nyuma kwa bao 1-0 kwa bao la Rodrigo.
Kipindi cha pili, Ufaransa iligeuka mbogo na kusawazisha dakika ya 49 kupitia Sunu na Alexandre Lacazette akafunga bao la ushindi dakika ya 85.

No comments:

Powered By Blogger