Sunday 25 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Guti aondoka Real baada ya Miaka 25
Kiungo wa Real Madrid Guti ametangaza anahama Real Madrid baada ya kuwa na Timu hiyo tangu Mwaka 1985 akiwa Timu ya Vijana na kisha kuitumikia Timu ya Kwanza kwa Miaka 15.
Guti, Miaka 33, amebakiza Mwaka mmoja kwenye Mkataba wake na Real lakini sasa anafikiria kuhamia huko Uturuki.
Guti amesema amepewa ofa nzuri na Besiktas ya Uturuki.
Katika Kikosi cha sasa cha Real Madrid, ni Raul pekee ndie aliedumu hapo muda mrefu kupita Guti.
Rio nje hadi mwishoni Agosti
Beki wa Manchester United, Rio Ferdinand, atalazimika kuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu kupita ilivyokadiriwa na sasa anategemewa kurudi tena mwanzoni mwa Septemba badala ya katikati ya Agosti.
Meneja wa Man United, Sir Alex Ferguson, ametoboa: “Rio atarudi baada ya Wiki 6.”
Kuchelewa kurudi kwa Rio kutamfanya pia azikose mechi za England za kuwania kufuzu kuingia Fainali za EURO 2012 zitazochezwa Septemba dhidi ya Bulgaria na Uswisi.
Pia atazikosa mechi za Ligi Kuu za Man United v Newcastle hapo Agosti 16, hii ikiwa mechi ya ufunguzi, na zile zinazofuata za Agosti 22 dhidi ya Fulham na Agosti 28 na West Ham.
Ferdinand aliumia goti huko Afrika Kusini mazoezini kwenye Kikosi cha England kilichokuwa kipo kwa Fainali za Kombe la Dunia na alipata maumivu hayo baada ya kugongana na Emile Heskey.
Fergie furahani
Wakati huo huo, Sir Alex Ferguson ameonyesha kufurahishwa kwake kwa Beki wake Nemanja Vidic kukubali kusaini Mkataba mpya.
Fergie ametamka: “Siku hizi ni ngumu kuwafanya Wachezaji wazuri kusaini Mkataba mpya na hasa Wachezaji watokao nje ya England. Kumekuwa na uvumi mwingi kuhusu Vidic. Tumefurahi amesaini tena! Yeye ni Sentahafu mzuri sana!”

No comments:

Powered By Blogger