Saturday 24 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Drogba kuukosa mwanzo Msimu Mpya
Straika wa Chelsea, Didier Drogba, ataukosa mwanzo wa Msimu mpya huko England baada ya kufanyiwa Operesheni ya nyonga yake iliyokuwa ikimsumbua toka mwishoni mwa Msimu uliokwisha.
Drogba, Miaka 32, alichelewesha kufanya operesheni hiyo ili aiwakilishe Nchi yake Ivory Coast Fainali za Kombe la Dunia lakini akakumbwa na kuvunjika kiwiko cha mkono wa kulia kabla ya Fainali hizo na ilibidi acheze huko Afrika Kusini huku amevaa gamba gumu kuulinda mkono huo alipopewa kibali maalum na FIFA kulivaa gamba hilo.
Inakadiriwa Drogba atakuwa nje ya uwanja kwa Wiki 3 na ataikosa mechi ya fungua pazia kugombea Ngao ya Hisani hapo Agosti 8 Uwanjani Wembley Chelsea watakapoivaa Manchester United.
Licha ya Drogba, Chelsea pia itawakosa kwa Wiki kadhaa mwanzo wa Msimu mpya Kipa Petr Cech, Difenda Alex na Mchezaji mpya Benayoun kwani wote ni majeruhi.

No comments:

Powered By Blogger