Monday 19 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Cole ni Liverpool!!!
Joe Cole atakuwa Mchezaji mpya rasmi wa Liverpool kwa Mkataba wa Miaka minne endapo atapita upimwaji wa afya yake unaotegemewa kufanyika katika Masaa 48 yajayo baada ya pande zote mbili kufikia makubaliano.
Cole amekuwa Mchezaji huru tangu mwanzoni mwa Mwezi huu baada ya Mkataba wake huko Chelsea, ambako alidumu Miaka 7, kumalizika bila ya maelewano ya kuundeleza.
Mchezaji huyo mwenye umri wa Miaka 28 alitua Chelsea akitokea West Ham Mwaka 2003.
Habari za Joe Cole kujiunga na Anfield zimethibitishwa na tovuti ya Liverpool.
Jol kutinga Fulham
Martin Jol anategemewa kutajwa kuwa ndie Meneja mpya wa Fulham kuchukua nafasi ya Roy Hodgson ambae amehamia Liverpool.
Jol, Miaka 54, ni Kocha wa Ajax ya Uholanzi kwa sasa na aliwahi kuifundisha Tottenham kati ya Mwaka 2004 na 2007.
Fulham imekuwa ikihusishwa na kuwachukua Kocha wa Ivory Coast Sven-Goran Eriksson, Kocha wa USA Bob Bradley na hata Kocha wa Uswisi Ottmar Hitzfield lakini kuna kila dalili nafasi hiyo imetwaliwa na Martin Jol ambae leo anategemewa kujiunga na Msafara wa Timu ya Fulham kwenda kwenye ziara ya Siku 10 huko Sweden kwa ajili ya maandalizi ya Msimu mpya.

No comments:

Powered By Blogger