Friday 23 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Liverpool wapata Mpinzani EUROPA LIGI
Liverpool watakutana na Ranotnicki ya Macedonia kwenye Raundi ya 3 ya Mtoano ya EUROPA LIGI baada ya Timu hiyo ya Macedonia kutoka sare 0-0 na Mirka ya Armenia.
Rabotnicki iliifunga Mirka 1-0 mechi ya kwanza.
Liverpool watacheza mechi ya kwanza na rabotnicki Julai 29 Uwanja wa Anfield na marudio ni Agosti 5 huko Macedonia.
Wakati huohuo, UEFA imeitoa Klabu ya Spain, Mallorca, kwenye Mashindano ya EUROPA LIGI baada ya Klabu hiyo kukumbwa na madeni.
Mallorca imepewa siku 3 kukata rufaa.
Riera kuhamia Olympiakos
Mchezaji wa Liverpool, Riera, amekwenda Ugiriki kukamilisha taratibu za kuhamia Olympiakos.
Riera, Miaka 28, alijiunga Liverpool Mwaka 2008 akitokea Espanyol ya Spain na anategemewa kusaini Mkataba wa Miaka mitatu na Olympiakos.
Vidic kuongezewa Mkataba Man United
Manchester United inategemewa kuuboresha na kuongeza Mkataba wa Beki wao Nemanja Vidic licha ya kuandamwa na uvumi kuwa yuko mbioni kwenda Real Madrid.
Hivi juzi Sir Alex Ferguson alishindwa kuwahakikishia Wanahabari hatma ya Vidic alipokuwa anahojiwa.
Inategemewa Vidic, Miaka 28, ataongezewa Miaka miwili kwenye Mkataba wake unaoisha 2012 na pia Mshahara kupanda kutoka Pauni 70,000 hadi 90,000 kwa wiki.
Vile vile, Sir Alex Ferguson amethibitisha Chipukizi Danny Welbeck na Tom Cleverly, wenye Miaka 20 na 19, watakopeshwa kwa Timu nyingine za Ligi Kuu kwa Msimu ujao ili kuwapa nafasi ya kucheza mechi nyingi na kupata uzoefu zaidi.
Sunderland imeshaonyesha nia ya kumchukua Welbeck.
Milner kuhama Villa
Aston Villa imenyoosha mikono kwa Mchezaji wao James Milner ambae ametaka kuihama Klabu hiyo huku Manchester City ikiwa ndio safari yake.
Martin O’Neill, Meneja wa Villa, meungama kuwa Milner ataondoka lakini kwa dau wanalotaka wao ambalo linakadiriwa kuwa ni Pauni Milioni 30.
Aston Villa walikuwa tayari kuuboresha Mkataba wa Milner na kumfanya awe Mchezaji anaelipwa bora kupita wote hapo lakini mwenyewe ameng’ang’ania kuhama.

No comments:

Powered By Blogger