Thursday 22 July 2010

PITIA: www.sokainbongo.com

Mvutano kufanya Afrika Kusini isiitwe Bafana Bafana
Wakati kila Mtu anatambua jina Bafana Bafana ni jina maarufu ambalo kila Mtu amelizoea kuwa ni jina la Timu ya Taifa ya Soka ya Afrika Kusini, huenda jina hilo lisitumike tena kuitambua Timu ya Afrika Kusini baada ya kuzuka mzozo mkubwa uliotinga hadi Mahakama Kuu ya Rufaa ya Afrika Kusini na sasa kuelekea Bungeni mwa Nchi hiyo.
Zozo hilo limelipuka baada ya Mfanyabiashara mmoja kupata hatimiliki za jina Bafana Bafana Mwaka 1994.
Ingawa Chama cha Soka cha Afrika Kusini, SAFA, kiliendelea kuiita Timu yao ya Taifa Bafana Bafana lakini hawakuruhusiwa kutumia jina hilo kwenye biashara ya aina yeyote na ndipo gomvi hilo likaangukia Mahakamani Mwaka 1997 na hatimae kuishia Mahakama Kuu ya Rufaa ambako SAFA kilishindwa.
Inasadikiwa Mfanyabiashara mwenye kumiliki jina hilo la Bafana Bafana alivuna kiubwete, bila jasho, faida ya Pauni Milioni 6.5 wakati wa Fainali za Kombe la Dunia zilizoisha hivi karibuni, kwa matumizi ya jina hilo.
Jina la Bafana Bafana, likimaanisha ‘Vidume Vidume’, lilibuniwa na Wanahabari wa Soweto Miaka ya 1990 mara tu baada ya Afrika Kusini kuruhusiwa tena kushiriki Mashindano ya Kimataifa baada ya sera dhalimu za ubaguzi kuuliwa.
Rais wa SAFA, Kirsten Nematandani, amelalama: “Sipendi kusema tuna hasira kuhusu hilo! Tuna wasiwasi kwamba ingawa jina la Bafana Bafana ni rasilimali ya Taifa lakini huenda likabadilika!”

No comments:

Powered By Blogger