Wednesday 21 July 2010

SOMA PIA: www.sokainbongo.com

Kipa Cech aumia, nje Wiki 4
Kipa Nambari Wani wa Mabingwa wa Ligi Kuu England, Petr Cech, ataukosa mwanzo wa Msimu mpya baada ya kuumia mguu mazoezini hapo jana Jumanne na atakuwa nje kwa Mwezi mmoja.
Uchunguzi wa kina umethibitisha kuwa amechanika musuli za mguu wake wa kulia.
Chelsea wana Makipa wengine wawili, Ross Turnbull na Henrique Hilario.
Mechi ya kwanza kwa Msimu mpya kwa Chelsea ni ile mechi ya kugombea Ngao ya Hisani hapo Agosti 8 watakapocheza na Manchester United Uwanja wa Wembley na wataanza kampeni yao ya kutetea Ubingwa wa Ligi Kuu hapo Agosti 14 watakapocheza na West Bromwich Albion, Timu ambayo imepanda Daraja Msimu huu.
Degen ruksa kuondoka Liverpool
Meneja mpya wa Liverpool Roy Hodgson amemwambia Beki Philipp Degen yuko huru kuhama Klabi hiyo ikiwa atapenda.
Degen, Beki wa Kimataifa wa Uswisi mwenye Miaka 27, alitua Liverpool Julai 2008 akitokea Borussia Dortmund, ameanza mechi 8 tu na kuingizwa toka benchi mechi 5 tu katika muda wote akiwa Liverpool.
Hodgson ametamka: “Tumekuwa nae kwenye mazungumzo mazuri na tumekubaliana yuko huru kutafuta Klabu nyingine.”
Hodgson yuko mbioni kuisuka upya Liverpool na tayari ameshawanasa Wachezaji wapya wawili, Fowadi wa England Joe Cole na yule wa Serbia Milan Jovanovic, na pia wameshakubaliana na Rangers ya Scotland kumsaini Beki Chipukizi Danny Wilson.
Vilevile, Hodgson amepata uhakika wa Nahodha Steven Gerrard kubakia Liverpool baada ya kufanya nae mazungumzo kufuatia uvumi kuwa anataka kuondoka.
Sasa Hodgson atakuwa akiomba Mastaa wake wawili, Fernando Torres na Javier Mascherano, watafuata nyayo za Gerrard.

No comments:

Powered By Blogger