Sunday 18 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Liverpool kumuuza Insua
Liverpool wamekubaliana na Klabu ya Italia Fiorentina ili kumuuza Fulbeki wao Emiliano Insua na tayari Beki huyo ameshaondoka kambi ya mazoezi huko Uswisi walikokuwa wakijitayarisha kwa Msimu mpya kwenda Italia kujadiliana na Fiorentina kuhusu maslahi yake binafsi.
Insua, Miaka 21, alijunga Januari 2007 akitokea Klabu ya kwao huko Argentina Boca Juniors na ameichezea Liverpool mechi 62 na kufunga bao moja.
Liverpool watalazimika kutafuta Beki wa kushoto baada ya Fabio Aurelio nae kuhama Mwezi Juni.
Wenger ataka wamkome Fabregas!
Arsene Wenger anategemea uvumi na maneno kwamba Nahodha wake hapo Arsenal, Cesc Fabregas, anahamia FC Barcelona sasa utakoma baada ya yeye na Fabregas kukutana na kufanya mazungumzo.
Arsenal tayari wameshaikataa ofa ya Barca na hivi juzi Rais wa Barca, Sandro Rosell, alionekana kukiri kushindwa kwao kumtoa Fabregas Arsenal.
Ingawa Wenger amegoma kutoboa nini alizungumza na Fabregas lakini amesema: “Kumekuwa na mengi yamesemwa! Siku zote nimekuwa nikisema Fabregas ni Nahodha wetu na ni Mtu muhimu kwetu! Tunataka abaki na ndio maana hatutaki kusikiliza ofa yeyote.”
Terry kulikwaa shoka la Capello
Nahodha wa zamani wa Italia, Fabio Cannavaro, ambae anamjua vyema Kocha wa England, Fabio Capello, ambae ni Mtaliana mwenzake, amedai John Terry hataendelea tena kuchezea England chini ya Capello.
Terry alikwaruzana na Capello huko Afrika Kusini kwenye Fainali za Kombe la Dunia wakati alipodai Wachezaji wa England wako tayari kumhoji Capello kuhusu mbinu na uteuzi wa Timu na Capello akajibu kwa kudai Terry anafanya ‘kosa kubwa’ lakini hakumtema na England wakatupwa nje ya Kombe la Dunia walipopigwa 4-1 na Germany.
Cannavaro, aliewahi kufundishwa na Capello huko Real Madrid, amesema: “Mawazo yangu ni kuwa Terry hawezi kuwamo tena kwenye England ya Capello!”
Cannavaro akaongeza: “Huwezi kumkosa Fabio na akakutazama tu!”
Pia, Cannavaro amedai kuwa katika Kikosi cha England kilichocheza na kufungwa na Germany huko Afrika Kusini hadhani kama zaidi ya Wachezaji watano watabakia kwenye Timu ya baadae ya Capello na amesema ni Wachezaji wawili tu ndio wenye uhakika wa kuwemo kwenye Kikosi cha England na hao akawataja ni Ashley Cole na Wayne Rooney.

No comments:

Powered By Blogger