Saturday 17 July 2010

TEMBELEA: www.sokainbongo.com

Arsenal, Chelsea zashinda mechi za kujipima
Katika mechi za kirafiki na za matayarisho kwa ajili ya Msimu mpya, leo Chelsea na Arsenal zilicheza na kushinda mechi zao.
Chelsea iliifunga Crystal Palace kwa bao 1-0 kwa bao lililofungwa na Michael Essien kwenye dakika ya 60.
Nao Arsenal waliichabanga Barnet FC kwa bao 4-0 na hadi mapumziko Arsenal walikuwa mbele kwa bao 3-0.
Mabao ya Arsenal yalifungwa na Andre Arshavin, dakika ya pili, Simpson, mabao mawili dakika za 16 na 45, na Samir Nasri akafunga dakika ya 75.

No comments:

Powered By Blogger