Saturday 17 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Mascherano hana mawasiliano na Liverpool
Meneja mpya wa Liverpool, Roy Hodgson, amesema hana mawasiliano na Kiungo wao Javier Mascherano ambae kwa sasa yuko likizo baada ya kutoka Afrika Kusini kwenye Kombe la Dunia alipokuwa na Nchi yake Argentina.
Hodgson amekuwa akitaka kuongea na Mascherano hasa kwa vile kumekuwa na uvumi mkali anataka kuhama kwenda Inter Milan kuungana na aliekuwa Meneja wa Liverpool, Rafael Benitez.
Pia inadaiwa Klabu nyingine kama vile Chelsea, Manchester City na FC Barcelona zinamuwinda.
Hodgson amesema: “Nimejaribu kuwasiliana na Mascherano lakini hapatikani kwa simu na pia hajibu ujumbe wa simu.”
Mascherano ana Mkataba na Liverpool hadi 2012.
Wakati huo huo, Hodgson amesema ameshakutana na kuongea na Steven Gerrard na Fernando Torres na Wachezaji hao hawauzwi.
Kumekuwa na uvumi pia kuwa Mastaa hao wawili wanataka kuondoka.
Makamu Mwenyekiti wa Kanisa hilo, Win Bijman, amesema: “Watu hawaelewi kwa nini amesimamishwa. Kanisa hapa linajaa kwa ajili yake na Makanisa mengine ni matupu!”
Hata hivyo, sala za Padre Paul Vlaar hazikupokewa kwani Holland ilifungwa 1-0 na Spain waliotwaa Kombe la Dunia.

No comments:

Powered By Blogger