Sunday 11 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

PWEZA PAULO AENDELEZA LIBENEKE!!
Utabiri wa Pweza aitwae Paulo alie huko Oberhausen, Ujerumani umeendelea kutimia pale Germany walipoifunga Uruguay mabao 3-2 hapo jana Jumamosi, Julai 10 na kutwaa nafasi ya 3 kwenye Kombe la Dunia 2010.
Lakini macho ya Dunia nzima yapo kwenye mechi ya leo ya Fainali ya Kombe la Dunia kati ya Holland na Spain ambayo Pweza Paulo ameshatabiri kuwa Mshindi ni Spain.
Je Pweza Paulo ataendeleza libeneke?
Fergie akanusha kumtaka Sneijder!!
Bosi wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, amezikataa ripoti kwamba wametoa ofa kwa Inter Milan ili kumnunua Wesley Sneijder ambae anang’ara mno kwenye Kombe la Dunia huko Afrika Kusini akiwa na Nchi yake Uholanzi ambayo leo inacheza Fainali na Spain.
Ripoti hizo pia zilimnukuu Rais wa inter Massimo Moratti akidai ni kweli Man United inamtaka Sneijder.
Hata hivyo Ferguson ametamka: “Sijui ripoti hizo zinatoka wapi! Inawezekanaje waikatae ofa yangu wakati sijatoa ofa yeyote? Kwanza nina Kikosi kizuri tu na Vijana wangu wadogo sasa wamepata uzoefu wa Mwaka mmoja zaidi tangu Msimu uliopita!”
Ferguson pia amekanusha ripoti kuwa baada ya kukataliwa Sneijder sasa anataka kumchukua Kiungo wa Germany Mesut Ozil ambae pia aling’ara huko Afrika Kusini kwenye Kombe la Dunia.

No comments:

Powered By Blogger