Thursday 15 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Heskey ang’atuka England
Straika wa Aston Villa Emile Heskey ametangaza kustaafu kuichezea Timu ya England.
Mchezaji huyo mwenye Miaka 31, aliechezea England mara 62 na kufunga goli 7 tu, alikuwemo Kikosi cha England huko Afrika Kusini kwenye Kombe la Dunia na kucheza mechi ya kwanza dhidi ya USA na ile na Algeria kisha kupigwa benchi mechi na Slovenia.
Hata hivyo uteuzi wake kwenye Kikosi hicho cha England ulizua mshangao kwa vile Msimu mzima uliopita akiwa na Aston Villa alifunga bao 3 tu.
Fergie adai Wachezaji watarudi bila ‘hengiova’
Bosi wa Manchester United Sir Alex Ferguson amesema haamini kuwa Wayne Rooney na wenziwe waliocheza bila mafanikio Kombe la Dunia huko Afrika Kusini watarudi Klabuni wakiwa na ‘hengiova’ ya kutofanya vizuri kwenye Mashindano hayo makubwa.
Rooney alikuwa na England huko Afrika Kusini lakini hakung’ara na hakufunga hata bao moja katika mechi nne alizocheza ya mwisho ikiwa kipigo cha 4-1 toka kwa Germany.
Wachezaji wengine wa Man United waliokuwa kwenye Kombe la Dunia ni Michael Carrick [England], Patrice Evra [France], Nemanja Vidic [Serbia], Park Ji-sung [South Korea] na Javier ‘Chicharito’ Hernandez [Mexico].
Wachezaji hao wote wataripoti tena Julai 28 wakitokea likizo.
Ferguson amesema: “Sitegemei huzuni na kuvunjika moyo toka kwao. Watahisi wamekosa kitu lakini hawataathirika.”
Lakini Ferguson akasema anahisi Mchezaji pekee ambae ataridhika na uchezaji wake huko Afrika Kusini ni Mchezaji mpya Chipukizi Hernandez aliechezea Mexico na kufunga bao mbili.
Wigan yamchota Kipa Al Habsi
Wigan Athletic imemsaini Kipa wa Kimataifa wa Oman Ali Al Habsi kwa mkopo wa Mwaka mmoja kutoka Bolton Wanderers.
Kipa huyo mwenye Miaka 28 amekuwa hana namba huko Bolton lakini katika mechi chache alizocheza amekuwa akifanya vizuri na Kocha wa Wigan, Roberto Martinez, amesema Al Albsi ataleta ushindani kwa Kipa wao Nambari Wani Chris Kirkland.
Al Absi ameichezea Oman mara 70 katika mechi za Kimataifa.
Wigan imekuwa haina Makipa wa Akiba baada ya kuondoka kwa Richard Kingson na Vladimir Stojkovic.
Wigan watacheza mechi yao ya kwanza ya Ligi Kuu England kwa Msimu mpya wakiwa nyumbani DW Stadium dhidi ya Blackpool, Timu ambayo imepanda Daraja.

No comments:

Powered By Blogger