Sunday 11 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Kiatu cha Dhahabu Kombe la Dunia: Leo Mshindi ni Villa au Sneijder?
Leo ni kitimtim cha nani atakuwa Bingwa wa Dunia kati ya Holland na Spain zitakazokwaana kuanzia saa 3 na nusu usiku [bongo] huko Uwanja wa Soccer City, Soweto, Johannesburg lakini pia kwa Wachezaji kuna kitimtim cha nani atatwaa Kiatu cha Dhahabu kwa kuwa Mfungaji Bora wa Kombe la Dunia 2010.
Ingawa kuna Wachezaji wanne wamefungana juu kwa kufunga bao 5 kila mmoja lakini wenye nafasi kubwa ya kunyakua Tuzo hii, kwa vile Timu zao zinacheza leo, ni David Villa wa Spain na Wesley Sneijder wa Holland.
WAFUNGAJI BORA:
-Villa bao 5 [Spain]
-Sneijder bao 5 [Holland]
-Forlan bao 5[Uruguay]
-Muller bao 5 [Germany]
-Klose bao 4 [Germany]
-Higuain bao 4 [Argentina]
-Vittek bao 4 [Slovakia]
-Donovan bao 3 [USA]
-Gyan bao 3 [Ghana]
-Fabiano bao 3 [Brazil]
-Suarez bao 3 [Uruguay]
Klose akosa kuifikia rekodi ya Ronaldo
Miroslav Klose wa Germany jana alishindwa kuifikia rekodi ya Ronaldo de Lima wa Brazil ya kufunga jumla ya mabao 15 katika mechi za Fainali ya Kombe la Dunia.
Klose, mwenye jumla ya mabao 14, jana alishindwa kucheza mechi kutafuta Mshindi wa 3 wa Kombe la Dunia ambayo Germany iliifunga Uruguay kwa bao 3-2.
Klose alishindwa kuchezeshwa kwa vile alikuwa anakabiliwa na maumivu ya mgongo.
Germany 3 Uruguay 2
Sami Khedira alifunga bao la 3 na kuwapa Germany ushindi wa ba0 3-2 dhidi ya Uruguay na hivyo kunyakua ushindi wa 3 wa Kombe la Dunia huko Afrika Kusini.
Germany ndio walikuwa wa kwanza kupata bao pale shuti la Mita 30
la Schweinsteiger kutemwa na Kipa Fernando Muslera na kumwangukia Muller aliefunga.
Uruguay walisawazisha kupitia Edinson Cavani aliepokea pasi ya Suarez na dakika 6 ndani ya Kipindi cha Pili Forlan alifunga bao la pili baada ya pasi ya Suarez.
Germany wakasawazisha kwa kichwa cha Marcell Jensen baada Kipa Muslera kuikosa krosi.
Timu:
URUGUAY: 1-Fernando Muslera; 2-Diego Lugano, 3-Diego Godin, 4-Jorge Fucile, 16-Maximiliano Pereira, 15-Diego Perez, 17-Egidio Arevalo, 7-Edinson Cavani, 22-Martin Caceres, 9-Luis Suarez, 10-Diego Forlan.
GERMANY: 22-Hans-Joerg Butt; 2-Marcell Jansen, 3-Arne Friedrich, 17-Per Mertesacker, 20-Jerome Boateng, 13-Thomas Mueller, 4-Dennis Aogo, 6-Sami Khedira, 7-Bastian Schweinsteiger, 19-Cacau, 8-Mesut Ozil.
Refa: Benito Archundia (Mexico)

No comments:

Powered By Blogger