Saturday 17 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com
Man United 3 Celtic 1
Mabao ya Berbatov, Danny Welbeck na Tom Cleverly jana yamewapa ushindi Manchester United wa 3-1 dhidi ya Celtic ya Scotland Uwanjani Rogers Centre huko Toronto, Canada katika mechi yao ya kwanza ya ziara yao ya huko Canada, Marekani na Mexico.
Man United ndio walikuwa wa kwanza kupata bao Mfungaji akiwa Dimitar Berbatov dakika ya 34 kufuatia pasi ya Mame Biram Diouf.
Celtic walisawazisha kwa penalti ya Georgios Samaras dakika ya 61 baada ya Wes Brown kumwangusha Straika wa Celtic.
Danny Welbeck alifunga bao la pili dakika ya 74 baada ya kupokea pasi toka kwa Berbatov na dakika ya 86 Cleverly akapachika bao la 3 kwa shuti lililombabatiza Beki na kumbabaisha Kipa Lukasz Zaluska.
Kikosi cha Man United kilichoanza kilikuwa:
Edwin van der Sar, Ryan Giggs, Paul Scholes, Darren Fletcher, Berbatov, Fabio, Rafael, Jonny Evans, Smalling, Obertan, Diouf.
Mechi inayofuata kwa Man United ni huko Philadelphia, Marekani hapo Julai 21 dhidi ya Philadelphia Union.

No comments:

Powered By Blogger