Sunday 11 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Suarez aililia Ligi Kuu England!!
Mchezaji wa Ajax ya huko Uholanzi, Luis Suarez, ambae pia aliichezea Uruguay kwenye Kombe la Dunia huko Afrika Kusini na kujizolea sifa kubwa, nzuri na mbaya, amedai anapenda kucheza Ligi Kuu England hasa Manchester United au Tottenham.
Suarez, Miaka 23, Msimu uliokwisha aliifungia Ajax mabao 50 na kwenye Kombe la Dunia huko Afrika Kusini alipachika bao 3 kwa Uruguay lakini pia alijizolea sifa mbovu ya kuudaka mpira kwenye mstari wa goli dakika ya mwisho ya mechi na kuinyima Ghana ushindi wa wazi kitendo ambacho alitwangwa Kadi Nyekundu.
Huko nyuma Suarez aliwahi kuhusishwa na kuhamia Manchester United lakini mwenyewe amekiri huu ni wakati muafaka kuhamia England kwa jinsi Ligi Kuu ilivyokuwa na timu Bora.
Amesema: “Kuna Timu kama 5 zipo kiwango cha juu! Zitazame Man City na Liverpool zina kina Torres, Gerrard, Mascherano, Silva, Yaya Toure lakini hazimo UEFA CHAMPIONS LIGI!! Hii inaonyesha kuna Timu Bora huko!”
Suarez akamalizia: “Man United ni Timu bomba sana pamoja na Real Madrid na ndizo zinazosifika kupita zote Duniani! Unajua kabisa ukijiunga na Man United na kukaa kwa muda mrefu lazima utashinda Vikombe tu!”
Benayoun amponda Benitez
Kiungo wa zamani wa Liverpool Yossi Benayoun amemshambulia vikali aliekuwa Meneja wake huko Liverpool Rafael Benitez na kudai ndie aliesababisha yeye kuhama kwenda Chelsea.
Benayoun alidumu Liverpool Misimu mitatu lakini alikuwa akitumika kama Mchezaji wa Akiba.
Kiungo huyo amedai Benitez, ambae ameondoka Liverpool na sasa amejiunga na Inter Milan ya Italia, alimkosesha raha na alikuwa akimtendea vibaya.
Benayoun amesema: “Nikicheza vizuri hanipi pongezi, hata nikiingizwa na kafunga goli najua fika mechi ijayo sina namba! Msimu uliokwisha nilicheza mechi dhidi ya Fulham na ile na Lyon na akaamua kunibadilisha na Washabiki wakachukizwa na hilo na kuzomea! Yeye akadai nlicheza ovyo!”
Mchezaji huyo akaendelea kusema Benitez alikuwa akimwambia yeye ni Mchezaji mzuri akitokea benchi.

No comments:

Powered By Blogger