Tuesday 13 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Kombaini Bora ya Kombe la Dunia 2010 yatajwa
Mara baada ya Kombe la Dunia 2010 kumalizika kimetajwa Kikosi cha Wachezaji 11 Bora waliong’ara kwenye Kombe la Dunia huko Afrika Kusini na kinaundwa na Wachezaji watano kutoka kwa Mabingwa Dunia, Spain, watatu toka Germany na mmoja mmoja kutoka Holland, Ureno na Uruguay.
Kikosi kamili ni kifuatacho:
-Kipa: Iker Casillas [Spain]
-Beki wa Kulia: Sergio Ramos [Spain]
-Sentahafu: Arnie Friedrich [Germany]
-Sentahafu: Carles Puyol [Spain]
-Beki wa Kushoto: Fabio Coentrao [Ureno]
-Kiungo: Bastian Schweinsteiger [Germany]
-Kiungo: Xavi [Spain]
-Kiungo: Wesley Sneijder [Holland]
-Winga Kulia: Thomas Mueller [Germany]
-Winga Kushoto: Andres Iniesta [Spain]
-Straika: Diego Forlan [Uruguay]
Makocha wa Timu 32 za Kombe la Dunia 2010: WAPI WAENDA?
Fainali za Kombe la Dunia 2010 ndio hizo zimeaga hapo Jumapili Julai 11 kwa Spain kuifunga Holland 1-0 na kutwaa Ubingwa wa Dunia na baadhi ya Makocha walioongoza Timu 32 kwenye Fainali hizo tayari washang’oka, wengine kwa hiari na baadhi kwa kufukuzwa, huku wengine hawajui hatma zao.
Ifuatayo ni Listi yao na nini kimewajiri:
FRANCE: Raymond Domenech, baada ya kuiongoza France iliyokumbwa na migogoro na aibu huko Afrika Kusini, hayupo tena na nafasi yake imechukuliwa na Laurent Blanc.
ENGLAND: Fabio Capello bado yumo mzigoni ingawa England ilisulubiwa na Germany kwa bao 4-1 kwenye Raundi ya Pili ya Kombe la Dunia.
ITALY: Marcello Lippi, aliiongoza Italy kutwaa Kombe la Dunia 2006, lakini 2010 imetolewa Raundi ya Kwanza tu. Bado haijajulikana nini kitatokea kwake ingawa huenda akaondoka.
SLOVENIA: Matjaz Kek bado yumo mzigoni na nusura waingie Raundi ya Pili Kombe la Dunia kama si USA kuifunga Algeria dakika ya mwisho.
SLOVAKIA: Vladimir Weiss aliingiza Timu yake Raundi ya Pili na hiyo ni historia hivyo kubaki kwake si tatizo.
PORTUGAL: Carlos Queiroz amesema haondoki ingawa walitolewa Raundi ya Pili na Spain kwa bao 1-0 na ikafuata vita ya maneno kati yake na Cristiano Ronaldo.
SERBIA: Radomir Antic anabaki licha ya kushindwa kusonga mbele toka Raundi ya Kwanza.
HOLLAND: Bert van Marwijk aliipeleka Holland Fainali na kufungwa na Spain 1-0 na inasadikiwa bado atashika hatamu.
SPAIN: Ni lazima Vicente del Bosque atabaki kibaruani baada ya Spain kunyakua Ubingwa wa Dunia.
GERMANY: Mkataba wa Joachim Low umekwisha na hajaamua kama aendelee.
GREECE: Otto Rehhagel ameondoka baada ya kukaa Miaka 8 na kuisaidia Greece kunyakua EURO 2004 na kuiingiza EURO 2008 na Kombe la Dunia 2010 Mashindano ambayo yote walitolewa Raundi ya Kwanza tu.
USWISI: Ottmar Hitzfeld huenda akabaki na wao ndio Timu pekee iliyowafunga Spain huko Afrika Kusini.
DENMARK: Morten Olsen ana Mkataba hadi 2012.
GHANA: Milovan Rajevac huenda akaendelea na nusura aingize Ghana Nusu Fainali kama si mkono wa Luis Suarez wa Uruguay.
SOUTH AFRICA: Carlos Alberto Parreira anaondoka kwa vile Mkataba haupo tena.
CAMEROON: Paul Le Guen, ingawa anatakiwa abaki, pia Australia inamtaka na huenda akaondoka.
ALGERIA: Rabah Saadane bado anaheshimika huko Algeria na ni wazi hang’olewi labda atoke mwenyewe.
IVORY COAST: Sven-Goran Eriksson alikuwa na Timu hii kwa Mkataba wa muda mfupi tu.
NIGERIA: Lars Lagerback amepewa nyongeza ya Mkataba wa Miaka miwili.
AUSTRALIA: Pim Verbeek ameondoka.
NORTH KOREA: Licha ya kufungwa 7-0 na Ureno, kwa Kocha Kim Jong-Hun haijulikana ni nini kitamkuta sababu ya usiri wa Nchi hiyo.
SOUTH KOREA: Huh Jung-Moo amejiuzulu.
JAPAN: Takeshi Okada amejiuzulu.
NEW ZEALAND: Ricki Herbert bado yupo mzigoni kwa kuiwezesha Timu yake kutofungwa katika mechi 3 za Kundi lao walizotoka sare na kumaliza nafasi ya 3 juu ya Italy walioshika mkia.
USA: Bob Bradley ana uchu wa kuendelea na hamna presha kumng’oa.
HONDURAS: Reinaldo Rueda anaendelea.
MEXICO: Javier Aguirre ameamua mwenyewe kuondoka licha ya kutokuwa na shinikizo lolote la kumtoa.
BRAZIL: Dunga amefukuzwa.
ARGENTINA: Diego Maradona, licha ya kudharauliwa na Dunia juu ya uwezo wake kama Kocha, kwao ni kipenzi kikubwa na hivyo haitegemewi kuondolewa.
CHILE: Marcelo Bielsa atadumu.
URUGUAY: Oscar Tabarez aliipeleka Timu hadi kuchukua nafasi ya 4 na mwenyewe anataka kubaki.
PARAGUAY: Gerardo Martino yupo ofisini hadi baada ya Copa America Mwakani.

No comments:

Powered By Blogger