Friday 16 July 2010

CHEKI: http://www.sokainbongo.com/


UEFA CHAMPIONS LIGI: Droo Raundi ya 3 yatoka!!
Waliowahi kuwa Mabingwa wa Ulaya mara 4, AFC Ajax, wamepangwa kucheza na PAOK FC ya Ugiriki katika Raundi ya 3 ya Mtoano.
Celtic ya Scotland imepangwa kucheza na FC Braga ya Ureno.
Mechi za Raundi hii zitachezwa Julai 27 na 28 na marudio ni Agosti 3 na 4.
Droo inayofuata:
Droo hii itafanywa Agosti 6 ili kupata Timu zitakazocheza Raundi ya Mchujo kuingia kwenye Makundi na Droo hii itazijumuisha pia Timu za AJ Auxerre, Sevilla FC, Tottenham Hotspur FC, UC Sampdoria na Werder Bremen.
Mechi za Raundi hii ya Mchujo zitachezwa Agosti 17 na 18 na marudio ni Agosti 24 na 25.
Washindi 10 wa Raundi hiyo ya Mchujo wataungana na Timu 22 zitakazoingizwa moja kwa moja kwenye Droo ya kupanga Makundi 8 ya Timu nne nne kila moja.
Miongoni mwa Timu hizo 22 ni pamoja na Manchester United, Chelsea, Mabingwa wa Ulaya Inter Milan, Real Madrid, Bayern Munich, FC Barcelona na kadhalika.
Steji hiyo ya Makundi itaanza kuchezwa tarehe 14 na 15 Septemba na kumalizika Desemba 8.
Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI itachezwa Uwanja wa Wembley, London hapo tarehe 28 Mei 2011.
EUROPA LIGI: Droo ya Raundi ya 3 yatoka, Liverpool kilingeni!
Liverpool itaanza kinyang’anyiro cha kugombea UEFA EUROPA LIGI katika hatua ya Raundi ya 3 ya Mtoano na watakutana na Mshindi kati ya FK Rabotnicki ya Macedonia au FC Mika ya Armenia.
Mechi za Liverpool zitachezwa Julai 29 Uwanjani Anfield na marudiano ni Agosti 5 ugenini.
FK Rabotnicki wameifunga FC Mika 1-0 na marudio ni nyumbani kwa FC Mika huko Armenia.
Waliowahi kuwa Mabingwa mara mbili wa Ulaya, Juventus, wamepangiwa kucheza na Mshindi kati ya Timu ya Ireland Shamrock Rovers FC v Bnei Yehuda Tel Aviv FC ya Israel.
Nao Sporting Clube de Portugal watacheza na FC Nordsjaelland ya Denmark.
Droo inayofuata:
Washindi 35 wa Raundi ya 3 ya Mtoano wataunganishwa na Timu 15 zitakazotolewa Raundi ya 3 ya Mtoano wa UEFA CHAMPIONS LIGI pamoja na Timu nyingine 24 zikiwemo FC Porto, PFC CSKA Moskva, PSV Eindhoven na Aston Villa FC.
Hii itakuwa ni Raundi ya Mchujo kuingia kwenye Makundi na Droo yake itafanywa hapo Agosti 6.
Fainali ya EUROPA LIGI itachezwa Lansdowne Road, Dublin, Ireland hapo tarehe 18 Mei 2011.

No comments:

Powered By Blogger