Tuesday 13 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

FIFA yatoa Listi ya Ubora kwa Timu za Kombe la Dunia
FIFA imetangaza Listi ya Ubora kwa Timu 32 zilizocheza Fainali za Kombe la Dunia 2010 huko Afrika Kusini ambazo zilimalizika Jumapili Julai 11 kwa Fainali ya Holland v Spain na Spain kutwaa Ubingwa wa Dunia kwa kuifunga Holland 1-0.
Timu inayoshika Nambari Wani ni Spain, ikifuatiwa na Holland, Germany na Urugay.
Brazil wamechukua nafasi ya 6, Ghana ya 7 na England ya 13.
Akizungumzia kuhusu England na Brazil, Rais wa FIFA, Sepp Blatter, amesema: “England ndio Mama wa Soka, Brazil ndio moyo lakini siku hizi hakuna Taifa dogo kwenye Soka. Kuna Nchi ndogo lakini Timu zao za Taifa ni imara sana kwani Soka limepanda!”
Listi kamili:
1 Spain, 2 Netherlands, 3 Germany, 4 Uruguay, 5 Argentina, 6 Brazil, 7 Ghana, 8 Paraguay 9 Japan, 10 Chile, 11 Portugal, 12 United States, 13 England, 14 Mexico, 15 South Korea, 16 Slovakia 17 Ivory Coast, 18 Slovenia, 19 Switzerland, 20 South Africa, 21 Australia, 22 New Zealand, 23 Serbia, 24 Denmark, 25 Greece, 26 Italy, 27 Nigeria, 28 Algeria, 29 France, 30 Honduras, 31 Cameroon, 32 North Korea
Mastaa Man United kukosa mwanzo wa Ligi
Bosi wa Manchester United Sir Alex Ferguson amesema baadhi ya Wachezaji wake waliokuwa huko Afrika Kusini kwenye Kombe la Dunia huenda wakaikosa mechi yao ya kwanza ya Ligi Kuu na Newcastle hapo Agosti 16 kwa sababu wanatakiwa waanze mazoezi Julai 28 baada ya kupewa likizo.
Kikosi cha Wachezaji 22 cha Man United kipo Chicago kwa mazoezi na ziara ya mechi za kirafiki huko Marekani, Canada na Mexico, ziara ambayo inamalizika Julai 30.
Manchester United wanategemewa kucheza ile mechi ya kufungua pazia Msimu mpya kugombea Ngao ya Hisani na Mabingwa wa Ligi Kuu Chelsea Uwanjani Wembley, London hapo Agosti 8.

No comments:

Powered By Blogger