Tuesday 13 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Real haimtaki Gerrard, umri na bei vyawatisha!!
Real Madrid imesema haina nia ya kumchukua Nahodha wa Liverpool Steven Gerrard na hilo limetamkwa na Mshauri wa Ununuzi wa Wachezaji Ernesto Bronzetti.
Kumekuwa na tetesi kuwa baada ya Liverpool kukosa kucheza UEFA CHAMPIONS LIGI Msimu ujao, Gerrard hatabaki Liverpool na pia matamshi ya Meneja mpya wa Real Madrid, Jose Mourinho, kuwa anataka Wachezaji kama Gerrard kwenye Timu yake, yalileta dhana kuwa Gerrard yuko njiani kwenda Real.
Bronzetti amepasua kuwa Rais wa Real, Florentino Perez, hana nia na Gerrard kwa vile ana Miaka 30 na pia Liverpool wametaka dau kubwa la Pauni Milioni 58 kumuuza.
Redknapp asaini Mkataba mpya Spurs
Meneja wa Tottenham Harry Redknapp ameongeza Mkataba hadi 2013 kutoka uliopo sasa ambao ungekwisha Mwakani.
Redknapp, Miaka 63, akielezea hatua hiyo, alitamka: “Sasa Nipo Spurs kwa Miaka mitatu mingine na nina furaha! Nani anajua, naweza kukaa Miaka mingi zaidi!”
Meneja huyo alijiunga na Spurs akitoka Portsmouth Oktoba 2008 na Spurs ilikuwa ipo mkiani na akaipandisha hadi nafasi ya 8 lakini Msimu uliofuata, ule wa 2009/10 uliokwisha Mwezi Mei, aliiwezesha kumaliza nafasi ya 4, hivyo itacheza UEFA CHAMPIONS LIGI Msimu unaoanza Mwezi Agosti na hilo lilimfanya ateuliwa Meneja Bora wa Msimu wa Ligi Kuu England.
Akiongelea kuhusu kuongeza Mkataba wake, Redknapp alisema: “Hatujui nini kitatokea baadae lakini ukiwa bado na afya unaendelea. Ukiwaona Ferguson [Miaka 68], Capello [64], Wenger [60] na Roy Hodgson [62], unadhani naweza kufanya kama wao!”

No comments:

Powered By Blogger