Monday 12 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Mabingwa wa Dunia Spain watua kwao!
Kikosi cha Spain kikiwa na Kombe la Dunia kibindoni, baada ya kuifunga Holland 1-0 hapo jana Uwanjani Soccer City, Soweto, Johannesburg, leo mchana wametua Mjini Madrid, Spain.
Goli la Andres Iniesta la dakika ya 116 ndio limewapa Spain Ubingwa wa Dunia kwa mara ya kwanza katika histori yao.
Nahodha Iker Casillas akifuatana na Kocha Vicente del Bosque ndio walikuwa wa kwanza kushuka kwenye Ndege Uwanja wa Ndege wa Barajas huku Kundi kubwa la Watu likiwapokea.
Inategemewa Timu yote ya spain baadae itahudhuria sherehe kwa Waziri Mkuu wa Spain Jose Luis Rodriguez Zapareto.
Baada ya sherehe hizo Timu itazungushwa Mitaa ya Madrid ili Raia wawapokee na kuwashangilia Mashujaa wao.
Blatter aziponda Spain, Holland kwa uchezaji wa rafu!!
Rais wa FIFA, Sepp Blatter, amezilaumu Timu za Spain na Holland kwa kucheza mchezo wa rafu katika Fainali ya Kombe la Dunia hapo jana huko Johannesburg ambako Spain walitwaa Kombe kwa kuifunga Holland 1-0.
Mechi hiyo ilijaa rafu na mchezo usioridhisha uliomfanya Refa Howard Webb kutoka England aweke rekodi kwa kutoa Kadi 15 ikiwemo Nyekundu kwa Beki wa Holland Heitinga.
Blatter alilalamika: “Fainali haikuwa nilivyotegemea. Siwezi kuwalaumu Marefa kwani walikuwa na wakati mgumu mno kuchezesha na hawakusaidiwa na Wachezaji.”
Pia Blatter aliipongeza Spain kwa kuwa Mabingwa wa Dunia.
Forlan atwaa Mpira wa Dhahabu
Straika wa Uruguay Diego Forlan ametwaa Mpira wa Dhahabu kwenye Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini baada ya kuchaguliwa ndie Mchezaji Bora.
Forlan, Miaka 31, anaechezea Atletico Madrid na aliewahi kucheza Manchester United, alifunga bao 5 kwenye Fainali hizo na kuiwezesha Uruguay, bila kutegemewa, kufika Nusu Fainali.
Thomas Mueller, Miaka 20, wa Germany alishinda Tuzo ya Mchezaji bora Kijana.
Mueller pia alifunga bao 5.
Kipa na Nahodha wa Spain, Iker Casillas, ametwaa Tuzo ya Kipa Bora kwenye Fainali baada ya kufungwa bao mbili tu katika mechi 7 walizocheza huko Afrika Kusini.

No comments:

Powered By Blogger