Friday 16 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com
Barca wakata tamaa kwa Fabregas
Rais wa FC Barcelona, Sandro Rosell, amekiri huenda wasiweze kumchukua Cesc Fabregas kutoka Arsenal kabla Msimu mpya wa 2010/11 kuanza kwa vile Arsenal hawataki kusikia lolote kuhusu kumuuza Nahodha wao.
Rosell ametamka: “Arsenal wanaona kama wanaonewa. Hawataki kusikiliza ofa na wala kumuuza!”
Mwezi uliokwisha, Barca walitoa ofa ya Pauni Milioni 33 kumnunua Fabregas, mwenye umri wa Miaka 23 ambae alianza Soka akiwa mtoto kwenye Chuo cha Barca na kuhamia Arsenal akiwa na Miaka 16, lakini Arsenal waliikataa ofa hiyo.
Rosell alimaliza kwa kusema: “Atatua hapa kama si sasa ni baadae! Tutaona! Lakini hatuwezi kuwa wehu na kulipa pesa ambazo si thamani yake!”
Mkataba wa Fabragas Klabuni Arsenal unakwisha 2015.
Rooney kupandishiwa Mshahara
Mazungumzo ya kuuboresha Mkataba wa Wayne Rooney unaomalizika 2012 yatafanyika mapema Mwezi ujao baada ya Mkurugenzi Mtendaji wa Manchester United David Gill kurudi Manchester kutoka ziarani na Timu hiyo huko USA, Canada na Mexico.
Mazungumzo hayo yatafanyika kati ya Gill na Wakala wa Wayne Rooney, Paul Stretford.
Kwa sasa Rooney analipwa Pauni 90,000 kwa wiki na katika Mkataba mpya atakuwa akilipwa Pauni 130,000 kwa wiki na kumfanya awe ndie anaelipwa juu zaidi kupita Mchezaji yeyote hapo Manchester United.
Kabla, Cristiano Ronaldo, aliekuwa akilipwa Pauni 120,000, ndie alikuwa anaongoza akifuata Rio Ferdinand anaepata Pauni 110,000 kwa wiki.
Man City kumnasa Difenda toka Lazio
Manchester City wako mbioni kumchukua Beki wa Lazio kutoka Serbia, Aleksandar Kolarov, kwa Pauni Milioni 17.
Man City wanamtaka Fulbeki huyo wa kushoto anaesifika kucheza kama Gwiji Roberto Carlos ili pia kuchukua nafasi ya Wayne Bridge ambae Kocha Roberto Mancini anahisi si imara sana.
Huyo atakuwa Mchezaji wa nne kwa Man City kumnasa kabla Msimu mpya haujaanza wengine wakiwa David Silva toka Valencia, Yaya Touré toka Barcelona na Jerome Boateng kutoka Hamburg.
Inaaminika hao si Wachezaji wa mwisho kununuliwa kwani juhudi zipo za pia kuwabeba James Milner kutoka Aston Villa na Straika wa Wolfsburg ya Ujerumani, Edin Dzeko.

No comments:

Powered By Blogger