Wednesday 14 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Torres kukosa mwanzo wa Msimu
Baada ya Chama cha Soka cha Spain kuthibitisha kuwa Fernando Torres ameumia kiwango kikubwa kupita ilivyodhaniwa kwenye mechi ya Fainali ya Kombe la Dunia dhidi ya Holland, Liverpool wanangoja wamchunguze wenyewe lakini dalili zote zinaonyesha Straika huyo ataukosa mwanzo wa Msimu mpya wa Ligi Kuu England utakaoanza Agosti 14.
Liverpool imewapa Wachezaji wake wote waliocheza Kombe la Dunia likizo hadi mwanzoni mwa Agosti.
Torres amekuwa akiandamwa na majeruhi mfululizo Msimu uliokwisha ambapo aliumia musuli Mwezi Desemba Mwaka jana kisha akafanyiwa operesheni ya goti iliyomfanya asicheze Januari na Februari na ikafuata operesheni nyingine kwenye goti hilo hilo iliyomfanya azikose mechi 4 za mwisho za Ligi Kuu na Nusu Fainali ya EUROPA LIGI dhidi ya Atletico Madrid.
Hata hivyo, ingawa alikaa nje ya uwanja kwa wiki 6, Spain ilimchukua acheze Kombe la Dunia huko Afrika Kusini ambako alipwaya sana.
Kwenye mechi hiyo ya Fainali huko Johannesburg alingizwa toka benchi na kucheza dakika 10 tu na kuumia tena bila kuguswa na mtu.
Henry rasmi MLS USA
Thierry Henry amejiunga na Timu ya New York Red Bulls inayocheza Major League Soccer, MLS, huko Marekani akitokea FC Barcelona kwa Mkataba ambao utamzalishia Mamilioni.
Henry ameondoka Barcelona kama Mchezaji huru ingawa Mkataba wake ulibakiwa na Mwaka mmoja.
Henry, Miaka 32, huenda akacheza mechi yake ya kwanza kwa Red Bulls Julai 22 na Tottenham ya England kwenye mechi ya kirafiki.
LIGI YA MABINGWA CAF hatua ya Makundi
LIGI YA MABINGWA YA CAF ambayo ndio hutoa Klabu Bingwa Afrika inaendelea Wikiendi hii ikiwa inaingia hatua ya Makundi mawili yenye Timu 4 kila moja na Washindi wawili toka kila Kundi ndio wataingia Nusu Fainali.
KUNDI A lina Timu za:
-Esperance Sportive de Tunis [Tunisia]
-ES Setif [Algeria]
-TP Mazembe Englebert [Congo DR]
-Dynamos [Zimbabwe]
KUNDI B:
-El Ismaily [Egypt]
-El Ahly [Egypt]
-JS Kabylie [Algeria]
-HeartlandFC [Nigeria]
RATIBA:
Ijumaa Julai 16: ES setif v Esperance
Jumamosi Julai 17: Dynamo v Mazembe
Jumapili Julai 18: Heartland v El Ahly
El Ismaily v JS Kabylie
Ijumaa Julai 30: Mazembe v ES Setif

No comments:

Powered By Blogger