Thursday 15 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Maradona apewa dili mpya
Diego Maradona atapewa Mkataba mpya wa kuendelea kuifundisha Argentina hadi Fainali za Kombe la Dunia Mwaka 2014 zitakazochezwa huko Brazil.
Maradona aliifanikisha Argentina kufika Robo Fainali ya Kombe la Dunia huko Afrika Kusini hivi majuzi na kutolewa na Germany waliposhindiliwa bao 4-0.
Mwenyewe Maradona amekuwa akidokeza ataacha kuifundisha Argentina lakini Rais wa Chama cha Soka, AFA, Julio Grondona, amesema watakutana nae wiki ijayo ili wampe ofa ya Mkataba wa Miaka minne.
Licha ya Wadau wengi Duniani kumwona Maradona kama si Kocha stadi lakini huko kwao Argentina ni kipenzi kikubwa.
Rooney ashinda kesi
Wayne Rooney ameshinda kesi ya madai iliyokuwa ikimtaka alipe Pauni Milioni 4.3 kama fidia kwa kutolipa kamisheni ya mapato yake kwa Kampuni ya Proactive ambao waliwahi kuwa Wakala wake.
Jaji wa Mahakama ya Biashara huko Manchester, Jaji Brendan Hegarty, ametupilia mbali madai ya Proactive.
Proactive walikuwa wakimuwakilisha Rooney tangu 2002 wakati Mwanzilishi wa Kampuni hiyo, Paul Stretford, alipomsaini lakini Stretford alitoka Kampuni hiyo kwa ugomvi Mwaka 2008 na Rooney akaiacha Proactive na kuanza kuwakilishwa na Stretford binafsi.
Mwaka huo 2002, Stretford alipokuwa Proactive alipomsaini Rooney, Mchezaji huyo alikuwa na Miaka 17 na alikuwa akilipwa Pauni 80 kwa Wiki na Everton kwa vile alikuwa bado yupo kama Mwanafunzi Chuo cha Soka na alikuwa bado akiishi nyumba ya Serikali na Wazazi wake.
Lakini, Rooney akaibuka kuwa Staa na kuchukuliwa na Manchester United na kugeuka kuwa Milionea huku akiwa na Mikataba minono ya Matangazo ya Biashara na Kampuni kubwa kama Nike na Coca Cola.
Jaji Hegarty akitoa hukumu yake alisema Mkataba wa Rooney na Proactive ulikuwa ni Miaka minane na ni kinyume na FA ambao hutaka Mikataba kati ya Mawakala na Wachezaji iwe na kikomo cha Miaka miwili tu.
Baada ya hukumu hiyo, Rooney, ambae yuko Barbados vakesheni, alitoa tamko la kutoa shukrani zake na furaha yake kwa ushindi huo.

No comments:

Powered By Blogger