Thursday 22 July 2010

SOMA: www.sokainbongo.com

Fergie hajui kama Vidic anabaki
Bosi wa Manchester United Sir Alex Ferguson amekiri kuwa hana uhakika kama Beki wake Nemanja Vidic atakuwepo Man United Msimu ujao kwa vile kuna tetesi kubwa anaelekea Real Madrid.
Alipohojiwa, Ferguson alikataa kutoa ufafanuzi wowote licha ya kusema anaamini Beki huyo atabaki.
Kwa sasa Vidic na Wachezaji wenzake wengine waliokuwa kwenye Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini wamepewa likizo hadi Julai 28.
Hadi sasa hamna tamko lolote rasmi lililotolewa na upande wowote.
Fulham wamkosa Jol
Ajax Amsterdam imemtilia ngumu Meneja wake Martin Jol kuhamia Fulham licha ya Meneja huyo kutaka mwenyewe kuhama na pia kufikia makubaliano na Fulham kuhusu maslahi yake binafsi.
Fulham imekiri kumkosa Jol na imesema ipo mbioni kumsaka Mtu mwingine.
Kwa sasa Fulham haina Meneja baada ya Meneja wao Roy Hodgson kuhamia Liverpool.
Fulham pia imesema Kocha Msaidizi Ray Lewington ataendelea kuiendesha Timu hadi apatikane Meneja mpya.

No comments:

Powered By Blogger