Friday 23 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Fabianski Kipa Nambari Wani Ze Gunners?
Baada ya kutamka Kipa wake Manuel Almunia hukumbwa na mchecheto kwenye mechi kubwa na pia kumuwinda Kipa wa Fulham Mark Schwarzer, inaelekea Bosi wa Arsenal Arsene Wenger tayari ashambwaga Almunia na kumteua Lukasz Fabianski kuwa ndie Kipa Nambari Wani.
Kwenye mechi ya kujipima juzi Jumatano ambayo Arsenal walishinda 3-0 dhidi ya Sturm Graz, Fabianski ndie alieanza golini na Kipindi cha Pili akaingizwa mwenzake kutoka Poland Woiciech Szczesny.
Almunia, Miaka 33, aliidakia Arsenal mara 44 Msimu uliopita na aliwahi kuwa Nahodha wakati Cesc Fabregas alipokuwa majeruhi.
Henry afunga bao mechi ya kwanza na Red Bulls
Akicheza mechi yake ya kwanza tangu ajiunge na New York Red Bulls inayocheza MLS huko Marekani akitokea Real Madrid, Thierry Henry alifunga bao dakika ya 25 lakini hilo halikuweza kuiokoa Timu yake mpya kwani ilipigwa bao 2-1 na Tottenham Hotspur.
Mabao ya Tottenham yalifungwa dakika ya 62 na Robbie Keane na la pili na Gareth Bale dakika ya 72.
Mechi hii ilichezwa leo alfajiri Uwanja wa Red Bull huko New York, Marekani.
Mechi za Kirafiki Leo Julai 23:
Ajax Amsterdam v Chelsea
Deportivo la Coruna v FC Twente
Freiburg v Werder Bremen
Panathinaikos v West Ham
Manchester City v Sporting Lisbon

No comments:

Powered By Blogger