Saturday 24 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Ramalho agomewa na Fluminence, Brazil wampa ofa Menezes
Fluminense imekataa Kocha wao Muricy Ramalho aende kuifundisha Brazil na badala yake CBF, Shirikisho la Soka la Brazil, limempa ofa Kocha wa Corinthians, Mano Menezes, kuwa Kocha mpya wa Brazil kuchukua nafasi ya Dunga alietimuliwa.
Menezes, Miaka 48, amesema atatoa uamuzi wake baadae leo.
Inaaminika listi ya CBF ya Makocha ambao wanafaa kuwa Kocha wa Brazil wako Luiz Felipe Scolari, aliewahi kuifundisha Brazil, Ureno na Chelsea, Wanderley Luxemburgo, aliewahi kuwa Kocha wa Brazil, na Leonardo, aliekuwa Kocha wa AC Milan.

No comments:

Powered By Blogger