Monday 19 July 2010

PITIA: www.sokainbongo.com

FIFA yaanza ukaguzi wagombea Uenyeji 2018 & 2022
Wakaguzi wa FIFA leo wanaanza ziara yao itakayodumu Miezi miwili kuzikagua Nchi zilizoomba kuwa Wenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia Mwaka 2018 na 2022.
Fainali za Kombe la Dunia Mwaka huu zilifanyika huko Afrika Kusini na kumalizika Julai 11 na zile zinazofuata za Mwaka 2014 zitakuwa Brazil.
Wakaguzi hao watakuwa kila Nchi ya muombaji kwa Siku 3.
Ziara hiyo itaanzia Japan, Korea Kusini, Australia na kisha kwa waombaji wa pamoja Uholanzi na Ubelgiji, baadae England, na kwa waombaji wengine wa pamoja Spain na Ureno, kisha USA na halafu Qatar.
Timu hiyo ya Wakaguzi inaongozwa na Rais wa Shirikisho la Soka la huko Chile, Harold Mayne-Nicholls.
FIFA itatoa uamuzi nani watakuwa Wenyeji Mwaka 2018 na 2022 kufuatia mkutano wao huko Zurich, Uswisi Desemba 2, Mwaka huu.
RATIBA YA UKAGUZI:
-Julai 19-22: Japan [Wameomba 2022]
-Julai 22-25: Korea Kusini [Wameomba 2022]
-Agosti 9-12: Uholanzi & Ubelgiji [Waombaji wa pamoja]
-Agosti 16-19: Urusi
-Agosti 23-26: England
-Agosti 30-Septemba 2: Spain & Ureno [Waombaji wa pamoja]
-Septemba 6-9: USA
-Septemba 13-17: Qatar [Wameomba 2022]

No comments:

Powered By Blogger