Saturday 24 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Arsene na Arsenal yake
Arsene Wenger amesema Nahodha wake Cesc Fabregas atarudi kiwango chake cha kawaida ikifika Septemba mwaka huu kufuatia kuumia muda mrefu na kushiriki Kombe la Dunia huko Afrika Kusini ambako Nchi yake Spain ilitwaa Ubingwa wa Dunia.
Wenger ametamka: “Kimwili, ni bora kama hukucheza Kombe la Dunia kwani unapumzika lakini kiakili, ukicheza Kombe la Dunia, ni vigumu kupumzika na kurudi uko fiti Msimu mpya unapoanza.”
Cesc Fabregas na Robin van Persie wote walicheza Fainali ya Kombe la Dunia Julai 11 huko Afrika Kusini Nchi zao Spain na Holland zilipokutana na wote bado wako likizo hadi mwishomi mwa Julai.
Hata hivyo, Van Persie alikosa Miezi mitano ya Msimu uliokwisha kwa vile alikuwa majeruhi.
Huenda Fabregas na Van Persie wakacheza mechi yao ya kwanza kwa Arsenal hapo Agosti 7 huko Poland watakapocheza mechi ya kirafiki na Legia Warsaw, mechi ambayo ni ya wajibu kufuatia Mkataba wa Kipa wao Lukasz Fabianski kuwa na kipengele Arsenal icheze na Timu hiyo ya zamani ya Kipa huyo.
Kuhusu Theo Walcott na Samir Nasri, ambao wote hawakuchukuliwa na Timu zao za Taifa kwenda Kombe la Dunia Afrika Kusini, Wenger ametamka: “Sasa wapo na morali kubwa baada ya kuhuzunishwa kutocheza Kombe la Dunia. Siku zote Wachezaji kama hawa baada ya kuvunjika moyo hurudi uwanjani na ari mpya. Nasri yuko fiti mno!”
Juzi Samir Nasri aliifungia Arsenal bao 2 katika ushindi wa 3-0 dhidi ya Sturm Graz.
Arsene Wenger pia alitaja kuwa majeruhi wake, Denilson na Nicklas Bendtner, hawako katika hali mbaya sana.

No comments:

Powered By Blogger