Friday 23 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Wachezaji 23 wa Kombe la Dunia Ufaransa watemwa!
Kocha mpya wa Timu ya Ufaransa, Laurent Blanc, amekijulisha Chama cha Soka cha Ufaransa kuwa hatamwita hata Mchezaji mmoja kwa ajili ya mechi ijayo kati ya wale 23 walioiwakilisha Nchi hiyo kwenye Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini na kukumbwa na kashfa ya ugomvi, kufukuzwa kwa Nicolas Anelka, kogomea mazoezi na hatimae kubwagwa nje ya Mashindano hayo Raundi ya Kwanza tu huku wakiwa mkiani kwenye Kundi lao.
Ufaransa itacheza mechi ya kirafiki na Norway Mjini Oslo hapo Agosti 11 na hiyo itakuwa mechi ya kwanza chini ya Kocha Laurent Blanc.
Bramble ahamia Sunderland
Beki wa Wigan Titus Bramble amehamia Sunderland kwa Mkataba wa Miaka mitatu na kwa dau ambalo halikuanikwa.
Habari hizo zimethibitishwa na Kocha wa Sunderland, Steve Bruce, ambae alikuwa pamoja na Bramble huko Wigan alipokuwa Meneja wa Klabu hiyo.
Bruce ametamka: “Titus, nlipokuwa Wigan alikomaa na kuwa Mchezaji mzuri sana na sikusita katika kumleta Sunderland.”

No comments:

Powered By Blogger