Monday 19 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Giggs akiri Man United ni ya Vijana!
Mkongwe Ryan Giggs amekiri Manchester United ya Msimu wa 2010/11 uanzao Agosti 8 kwa mechi ya fungua pazia kugombea Ngao ya Hisani kati ya Mabingwa wa Ligi Kuu Chelsea na Manchester United Uwanjani Wembley Jijini London ni ya Chipukizi.
Giggs amesema Wachezaji wapya Chipukizi, Chris Smalling na Javier Hernandez, pamoja na Chipukizi waliojitokeza na kung’ara Msimu uliopita kama Nani, Antonio Valencia, Jonny Evans na Mapacha wa Brazil, Rafael na Fabio, ndio nafasi yao kuibeba Man United kwenye ushindi.
Giggs ametamka: “Msimu uliokwisha Wachezaji wengi Vijana walicheza Timu ya Kwanza. Nani alikuwa na Msimu mzuri, Valencia ulikuwa Msimu wake wa kwanza mzuri tu, Macheda alipata mbaya ya kuumia na sasa tumewapata Smalling na Hernandez!”
Giggs, ambae ameshashinda Mataji 11 ya Ligi Kuu akiwa na Man United, amedai kila Mchezaji hapo Old Trafford ana usongo wa kulirudisha Taji lao Klabuni hapo toka Chelsea.
Nae, Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, amefurahishwa na mchezo wa Difenda mpya Chipukizi Chris Smalling aliecheza mechi yake ya kwanza akiwa na Jezi ya Man United walipoifunga Celtic bao 3-1 huko Toronto, Canada hapo juzi.
Fergie ametamka: “Nimefurahishwa na uchezaji wake. Ni mwepesi na mtoaji pasi nzuri.”
Katika mechi hiyo ya kujipima nguvu, Smalling alicheza Sentahafu pamoya na Jonny Evans ikiwa ni mara yao ya kwanza kucheza pamoja.
CAF CHAMPIONS LIGI:
MATOKEO MECHI ZA MAKUNDI:
Julai 16: ES Setif [Algeria] 0 Esperance [Tunisia] 1
Julai 17: Dynamo [Zimbabwe] 0 TP Mazembe [Congo] 2
Julai 18:
Heartland [Nigeria] 1 El Ahly [Egypt] 1
El Ismaily [Egypt] 0 JS Kabylie [Algeria] 1

No comments:

Powered By Blogger