Wednesday 21 July 2010

SOMA TOVUTI: www.sokainbongo.com

UEFA CHAMPIONS LIGI kuwa na Marefa Watano 2011/12
IFAB [The International Football Association Board], ambao ndio wasimamizi wa kurekebisha sheria za Soka, wamesema UEFA CHAMPIONS LIGI mwakani itakuwa na Waamuzi watano Uwanjani, yaani Refa Mkuu, Washika Vibendera wawili na Wasaidizi wengine wawili ambao kila mmoja atakuwa nyuma ya goli moja.
Mtindo huo uklitumika kwenye mechi za EUROPA LIGI Msimu uliokwisha na pia utaendelea tena kwenye Mashindano hayo Msimu mpya wa 2010/11.
FIFA imesema majaribio ya Marefa hao watano katika mechi moja kwenye Mashindano makubwa kama ya UEFA CHAMPIONS LIGI na EUROPA LIGI yatawasaidia kufikia uamuzi Mwaka 2012 kama mtindo huo uwe wa kudumu.
Majaribio ya mtindo huo yanategemewa kuzagaa kwenye Mashindano makubwa katika Mabara ya Asia na Marekani Kusini.
Matukio ya utata na kusikitisha kwenye Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini hasa yale ya England kunyimwa goli la wazi kwa mpira kudunda Mita moja ndani ya goli na Refa kuwa kipofu katika mechi na Germany na lile la Ghana kufunga goli lilionekana kudakwa mstarini na Suarez wa Chile ndiyo yameiamsha FIFA kufikiria kubadili mitindo yake.
Mwezi Oktoba FIFA na IFAB zinategemewa kujadili kutumia teknolojia ya kisasa kwenye mstari wa goli ili kuwasaidia Marefa kutoa uamuzi wa uhakika na haraka kama mpira umevuka mstari au la.

No comments:

Powered By Blogger