Sunday 18 July 2010

PITIA: www.sokainbongo.com

Pique aonya: “Rooney ni Mbogo aliejeruhiwa!”
Mchezaji wa Mabingwa wa Kombe la Dunia Spain, Gerard Pique, anaechezea FC Barcelona, amewaonya wapinzani wa Manchester United kwenye Ligi Kuu kuwa Wayne Rooney atarudi Msimu mpya kama Mbogo aliejeruhiwa.
Pique, aliewahi kucheza na Rooney Man United kuanzia Mwaka 2004 hadi 2008 aliporudi tena Barcelona, amesema hajawahi kumwona Mchezaji akikasirika na kuumia moyo wakifungwa kama Rooney.
Pique ametamka: “Matokeo ya England huko Afrika Kusini na uchezaji wake utakuwa umemuumiza roho sana! Watu wanaweza kufikiri Wachezaji siku hizi wanalipwa pesa nyingi na haiwaumi wakifungwa lakini hebu wamtazame Rooney tu baada ya kufungwa kwenye chumba cha kubadilisha Jezi! Huwezi kuongea nae kwani ni kama Mtu anaeweza kulipuka dakika yeyote tu! Na Wachezaji wengi hupoa wikiendi baada ya mechi lakini Rooney hurudi Jumatatu akiwa na moto wa kulipiza kisasi! Hilo litawasaidia sana Man United!”
Kuhusu taarifa za Real Madrid na Klabu yake Barcelona kumtaka Rooney, Gerard Pique amesema hadhani kama Rooney atahama Man United kwa jinsi alivyokuwa na uhusiano mzuri na Meneja wake Sir Alex Ferguson.
Pique ametamka: “Rooney na Sir Alex ni kama Baba na Mwana! Sidhani kama Rooney atataka kuhama! Sir Alex ni Meneja mzuri mno na ni muungwana na mwema kwa kila Mchezaji! Lakini kwa Rooney, huyo ni kama Mtoto wake kipenzi!”

No comments:

Powered By Blogger