Friday 6 June 2008

Globaleyes==SAPOTA MAN U ABATUKA!
Haya tumeanza tena.
Mie ni nazi wa muda mrefu wa MAN U ambae nilimshabikia Ronaldo tangu alipotua Old Trafford akiwa mbavu za mbwa mpaka leo anaonekana mchezaji bora duniani aliefunga goli 42 kupita hata Alan Shearer alivyomudu maishani LIGI KUU.
Baada ya kutamka hivyo, ukweli ni kwamba leo mtizamo wangu kwake umebadilika. Msimamo na tabia yake siku hizi za karibuni zimenikera sana kwani amejionyesha yeye ni kama CD asiyekuwa hana hata chembe ya maadili ya kazi ya u-CD!
Na nikizungumza kama mtu nilieishi Spain, huo wenda wazimu wake wa kutaka kwenda Real unaonyesha kabisa hana akili. Angekuwa na akili kidogo tu agegundua Real ni mahala ambapo kumejaa wehu, wachezaji choka mbaya kiuchezaji, wala hongo, mafuska na wasiopendana huku uongozi wa klabu umenawiri ndumilakuwili, wanafiki, mafisadi na washenzi ambao labda ungewakuta katika Hekalu la Mfalme wa Karne ya 16. Au katika Klabu ya Chelsea ya sasa.
Akitaka kuhama- mwache ahame. Lakini kwanza agande na kuoza benchi mpaka Januari mwakani. Na asiondoke bila kulipwa Pauni za Kiingereza Milioni 100- isipungue hata ndururu!!!
Si wanamtaka basi yawatokee puani!!!

No comments:

Powered By Blogger