Thursday 5 June 2008

SHINAWATRA NA ERIKSSON
Mmiliki wa Manchester City Thaksin Shinawatra, ambae alikuwa Waziri Mkuu wa zamani wa Thailand, ametoa ufafanuzi kwanini alimtimua Sven Goran Eriksson kwa kudai Meneja huyo hakutoa mchango wa kutosha kuiinua timu.
Shinawatra alisema: 'Eriksson ni jemedari mzuri sana wa soka lakini tulikuwa tunataka zaidi. Lazima tucheze kwa ubora na uhakika zaidi. Awamu ya pili ya LIGI KUU tulikuwa dhaifu sana, tena sana! Tulibamizwa 8-1 na Middlesbrough katika mechi ya mwisho!!! Aibu, aibu kubwa!!!'
Shinawatra sasa amemwajiri aliekuwa Meneja wa Blackburn Rovers Mark Hughes kuendesha jahazi wakati Eriksson amevuka bahari ya Atlantic kwenda Mexico kuwa Kocha wa Timu ya Taifa ya nchi hiyo.

No comments:

Powered By Blogger