Sunday 1 June 2008



Ferguson aonya kuhusu Ronaldo
Bosi wa Manchester United Sir Alex Ferguson amesema klabu iko tayari Cristiano Ronaldo asicheze na badala yake akae vitini kama mtazamaji kuliko kumuuza kwa Real Madrid.
Man United tayari wameshatoa onyo kali kwa Real kuwa watawashitaki FIFA kwa kumrubuni Ronaldo kinyume na taratibu.
Ferguson amekutana na familia ya Glazer ambao ndio wanamiliki klabu na amesema:"Wao wana msimamo 'POTELEA MBALI NA TUKO TAYARI MCHEZAJI AKAE JUKWAANI KULIKO KUMUUZA'. Wako tayari kufanya hivyo ili kuonyesha msimamo kuwa sisi si klabu ya kuuza wachezaji wetu bora!'
Ronaldo, 23, kwa sasa yuko na kikosi cha Portugal kinachojitayarisha na Euro 2008 baada ya msimu bora ulioifanya Old Trafford iwe nyumbani mwa makombe ya LIGI KUU UINGEREZA na KLABU BINGWA BARANI ULAYA huku yeye akiwa ndio mfungaji bora katika Makombe yote mawili.

Mkataba wa Ronaldo unaisha 2012 na mwenyewe amesema ana furaha MAN U.
Baada ya onyo la MAN U kwa REAL kuwa watapelekwa FIFA, REAL walikuja hadharani na kutamka hawataki ugomvi na MAN U na hawawezi kumchukua mchezaji ambae klabu yake haitaki kumuuza.

********************************************************************************

TETESI NA UVUMI WA LEO..................................................

  • MAN U wako tayari na kitita cha pauni milioni 30 za Kiingereza kumnunua mshambuliaji chipukizi na mahiri wa LYON na Timu ya Taifa ya Ufaransa Karim Benzema.
  • Kiungo wa ARSENAL Alexander Hleb atajiunga na BARCELONA kwa dau la Pauni za Kiingereza milioni 12.
  • Mdogo wake Rio Ferdinand, mlinzi wa WEST HAM Anton Ferdinand yuko njiani kujiunga na TOTTENHAM.

No comments:

Powered By Blogger