Tuesday 3 June 2008



Mourinho aukwaa Umeneja Inter Milan!

Bosi wa zamani wa Chelsea Jose Mourinho ameteuliwa kuwa Meneja wa Klabu ya Serie A Inter Milan.
Mourinho amesaini mkataba wa miaka mitatu ikiwa ni kazi yake ya kwanza tangu atimuliwe Chelsea Septemba 2007.
Mourinho,45, anamrithi Roberto Mancini aliefukuzwa kazi majuzi mbali ya kuipa Inter Ubingwa wa Serie A mara tatu mfululizo ikiwa pamoja na msimu huu.
Mourinho atatangzwa rasmi leo saa 6 mchana mbele ya Waandishi habari.
**************************************************************************************

Nae Eriksson amwaga unga MAN CITY!!
Manchester City wamemtimua Meneja Sven-Goran Eriksson kwa amri ya mmiliki wa Klabu hiyo aliekuwa Waziri Mkuu wa zamani wa Thailand Thaksin Shinawatra mbali ya kuiwezesha timu hiyo kushika nafasi ya 9 katika LIGI KUU UINGEREZA.
Man City tayari washaomba kibali toka kwa Blackburn Rovers ili wafanye mazungumzo na Meneja wao Mark Hughes ili wakikubaliana ahamie Man City. Blackburn Rovers wamekubali ombi hilo na kuna uwezekano mkubwa Mark Hughes akahama.

No comments:

Powered By Blogger