Thursday 5 June 2008

GUMZO…uvumi na tetesi………za leo!!!!!

  • Meneja wa Roma Luciano Spalletti ameungana na Mtaliana mwenzake Carlo Ancelotti kukataa ofa ya kujiunga na Klabu ya Chelsea inayohaha kupata bosi mpya tangu wamtimue Avram Grant .


 

  • Nae Didier Drogba hayumo kwenye listi ya wanaotakiwa kwenda kumfuata Inter Milan Jose Mourinho kwani listi ya bosi huyo mpya haina mshambuliaje yeyote!


     

  • Juventus wameshaafikiana na kiungo wa Liverpool Xabi Alonso malupulupu yake binafsi ila kuna mvutano kati ya Klabu na Klabu kuhusu ada ya uhamisho huku Wekundu hao wakitaka Pauni za Kiingereza milioni 16 wakati Wataliana hao wako tayari kutoa Pauni milioni 14.5 za Kiingereza.


     


 


 

No comments:

Powered By Blogger