Tuesday 3 June 2008

TETESI NA UVUMI…………wa leo!!!!
=Manchester City wanahaha kumsaini Ronaldinho toka Barcelona na wako tayari kumlipa mshahara wa Pauni za Kiingereza laki £200,000-kwa wiki.


=Mourinho ambae ni Meneja mpya wa Inter Milan anataka kuwachukua wachezaji wake wa zamani toka Chelsea Ricardo Carvalho, Michael Essien and Frank Lampard kuwaleta Inter.


=Fabio Capello, Meneja wa Timu ya Taifa ya Uingereza, anasemekana atamchagua Nahodha wa kudumu wa Timu hiyo kati ya John Terry au Rio Ferdinand.


=Nicolas Anelka anajuta kwanini aliondoka Arsenal kujiunga na Real Madrid mwaka1999 na amesema ni bora angekuwa na Gunners kwa kipindi hiki chote.

No comments:

Powered By Blogger