Friday 6 June 2008


Mutu aamrishwa kuilipa Chelsea £9.6m
Mshambuliaji wa Romania Adrian Mutu ameamriwa na FIFA jana kuilipa Chelsea Pauni za Kiingereza milioni 9 na laki 6 kama fidia baada ya kugundulika ametumia madawa ya kulevya aina ya cocaine mwaka 2004 na hatimaye kufukuzwa klabuni hapo.
Chelsea walimnunua Mutu kutoka Parma mwaka 2003 kwa Pauni milioni £15 na kumtimua Oktoba 2004 baada ya kashfa hiyo ya madawa ya kulevya kugundulika na ambayo ilisababisha afungiwe miezi saba kucheza soka.
***************************************************************************************
Adebayor akanusha kuhama
Mshambuliaji wa kutegemewa wa Arsenal amekanusha habari zilizogaa kwamba yuko njiani kumfuata mchezaji mwingine aliehama Arsenal Mathieu Flamini na kujiunga na Klabu ya Serie A ya Italia Inter Milan.
Adebayor ametamka: 'Ni upuuzi mtupu kwani sihami na niko kwenye timu nzuri hapa na nina furaha. Tulikuwa na msimu mzuri na msimu ujao tutatwaa vikombe.'


*************************************************************************************
Barca wamuuza Giovani kwa Tottenham
Mchezaji wa miaka 19 Giovani raia wa Mexico amesaini mkataba wa miaka mitano na Tottenham Hotspurs kwa dau la Pauni za Kiingereza milioni 4 laki 7.
Giovani, ambae ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Kimataifa wa Brazil Zizinho alikulia Barcelona alipoaanzia timu ya watoto.

No comments:

Powered By Blogger