Wednesday 4 June 2008

Habari mpya 4 juni 2008





Hughes atua Man City kama Meneja

Mark Hughes ameteuliwa kuwa Meneja wa Manchester City kwa mkataba wa miaka mitatu kuchukua nafasi ya Eriksson aliefukuzwa juzi.
Mchezaji huyo wa zamani wa Manchester United na Chelsea alikuwa Meneja wa Blackburn Rovers kwa miaka mitatu na nusu na aliwezesha Blackburn kumaliza msimu uliopita wa LIGI KUU UINGEREZA kwenye nafasi ya saba. Vilevile, aliiwezesha Blackburn kufika Nusu Fainali ya Kombe la FA mara mbili mnamo miaka ya 2004 na 2007.***************

Sagna asaini mkataba mpya Arsenal
Beki wa kulia wa Arsenal Bacary Sagna amesaini mkataba mpya ambao Klabu hiyo wameuita wa muda mrefu.
Beki huyo mwenye miaka 25 alijiunga na the Gunners kutoka Auxerre ya Ufaransa mwanzoni mwa msimu uliopita na aliichezea Arsenal mechi 40 katika msimu wa 2007/08.



No comments:

Powered By Blogger