Wednesday 4 June 2008

GUMZO……uvumi na tetesi………………..za leo!!!!
Mameneja wa Kitaliana wa Roma Luciano Spalletti na wa Fiorentina Cesare Prandelli ni majina yaliyojitokeza kuchukua nafasi ya Umeneja iliyo wazi ya Klabu ya Chelsea baada ya Mtaliana mwingine Bosi wa AC Milan Carlo Ancelotti kutamka yeye atabaki AC Milan. Chelsea wanatafuta Meneja baada ya kumtimua Myahudi Avram Grant.

xxxxxxxxxxxx
Jose Mourinho, Bosi mpya wa Inter Milan, anasemekana amemuweka mlinzi wa Chelsea Ashley Cole kama mchezaji wa kwanza atakaemleta kwenye Klabu yake hiyo mpya. Itakumbukwa ni Mourinho aliemng’oa Ashley Cole Arsenal na kumpeleka Chelsea wakati alipokuwa Meneja wa Chelsea.
xxxxxxxxxxx


Winga wa Kireno Cristiano Ronaldo inadaiwa amesema ataihama Manchester United ndani ya mwaka mmoja na kutimiza ndoto yake ya kuhamia Real Madrid.
xxxxxxxxxx

Mark Hughes, Meneja wa sasa wa Blackburn Rovers, amefikia makubaliano ya mkataba wa miaka mitatu wenye thamani ya Pauni za Kiingereza milioni 9 ili kuwa Meneja mpya wa Manchester City.
xxxxxxxxxx
Hoteli moja mjini Manchester ina kilio baada ya kusikia Sven-Goran Eriksson anaondoka Man City kwenda Mexico kwani alikuwa anaingizia hoteli hiyo Pauni za Kiingereza £350,000 kwa mwezi kama gharama ya makazi yake ya kifahari hotelini hapo.
xxxxxxxxxx

Arsene Wenger amedai Arsenal itashinda kila kitu msimu ujao.


No comments:

Powered By Blogger