Sunday 27 December 2009

DAVID JAMES ataka kuhamia Spurs!
Kipa wa Portsmouth David James, miaka 39, ambae pia hudakia Timu ya England, ameonyesha dhamira yake ya kuungana tena na aliekuwa Meneja wa Portsmouth ambae sasa yupo Tottenham, Harry Redknapp, ili fufue matumaini yake ya kuitwa Kikosi cha England kitachokwenda Afrika Kusini kwenye Fainali za Kombe la Dunia mwakani.
James amesema: “Ni bora kuchezea Spurs, huko nafasi yangu ya kuchezea England itaongezeka! Harry ni Kocha bora na ndio maana Spurs wana mafanikio!”
Huko Tottenham, Kipa wao wa akiba, Carlo Cudicini, yupo nje baada ya kuumia kwenye ajali ya pikipiki na hilo litamfanya James awe Kipa Msaidizi chini ya Kipa kutoka Brazil Heurelho Gomes ambae siku za nyuma alionekana kupwaya.
Hata hivyo, Meneja wa sasa wa Portsmouth, Avram Grant, hayuko tayari kumwachia David James kuondoka ingawa anaweza kulazimika kumwachia kwa vile Portsmouth ina matatizo makubwa ya fedha.
LIVERPOOL yashinda kwa “msaada wa Refa!”
Jana Liverpool iliweza kuwafunga Wolves 2-0 kwenye Ligi Kuu baada ya Wolves kucheza mtu 10 mara baada ya Refa Andre Marriner kumtoa Stepen Ward kwa Kadi Nyekundu baada ya kumpa kadi ya pili ya Njano katika mazingira ya utatanisha.
Refa Marriner kwanza alimpa Kadi ya Njano Berra kwa rafu ambayo Ward alimchezea Lucas Leiva wa Liverpool lakini baada ya Wachezaji wa Liverpool kulalamika, Refa huyo aliongea na Msaidizi wake na ndipo alipompa Kadi ya Pili ya Njano Ward na kisha kumwonyesha Nyekundu na kumtoa.
Uamuzi huo uliwapa mwanya Liverpool waliofunga bao la kwanza kupitia Steven Gerrard na la pili akafunga Yossi Benayoun.
WOLVES walalamikia Refa kuibeba Liverpool!!!
Bosi wa Wolves Mick McCarthy amepinga vikali kutolewa Mchezaji wake Stephen Ward na Refa Andre Marriner ambae alimpa Kadi 2 za Njano na kisha Nyekundu na hivyo kuwapa mwanya Liverpool kupata bao 2 baada ya Wolves kubaki mtu 10.
Refa Marriner kwanza alimpa Kadi ya Njano Berra kwa rafu ambayo Ward alimchezea Lucas Leiva wa Liverpool lakini baada ya Wachezaji wa Liverpool kulalamika, Refa huyo aliongea na Msaidizi wake na ndipo alipompa Kadi ya Pili ya Njano Ward na kisha kumwonyesha Nyekundu na kumtoa.
McCarthy amedai: “Nimeona marudiao ya video! Sidhani alistahili kutolewa nje! Refa hakupata msaada wowote toka kwa Mwamuzi wa akiba Phil Dowd! Na pale alipompa KadI Berra na kulalamikiwa na Wachezaji wa Liverpool alilazimika kumpa Kadi Ward!! Hayo ni makosa kwa Refa kukubalisha presha ya Wachezaji!”
MANCINI aanza kibarua kwa ushindi!!
Meneja mpya wa Manchester CityRoberto Mancini ameanza kibarua kwa mguu mzuri baada ya kuwafunga Stoke City 2-0 hapo jana kwenye Ligi Kuu lakini amekiri kuwa Timu yake inabidi iongeze juhudi na kukaza uzi.
Mancini amembadili Meneja Mark Hughes Jumamosi iliyopita na mechi ya jana ilikuwa ndio mechi yake ya kwanza ambapo Martin Petrov na Carlos Tevez ndio waliomfungia mabao ya ushindi yaliyopatikana kipindi cha kwanza.
Wenger haitaki mipira ya kurusha!!
Arsene Wenger wa Arsenal amependekeza kuwa badala ya mipira kurushwa ikitoka pembeni mwa uwanja ziwe zinapigwa frikiki ili kuharakisha mchezo.
Mfaransa huyo pia amedai kuwa baadhi ya Timu kwenye Ligi kuu hunufaiki zaidi kwa vile tu wanao Wachezaji wenye nguvu ya kurusha mipira mbali na akatoa mfano wa Mchezaji wa Stoke City Rory Delap ambae akirusha mpira ni kama kaupiga kwa mguu na mara nyingi huipa ushindi Stoke kwa mipira ya kurusha.
Wenger amedai: “ Sheria ibadilishwe! Soka ni mpira wa miguu na si mikono!”

No comments:

Powered By Blogger