Wednesday 30 December 2009

Kigoli cha ‘babu’ chaipa ushindi Liverpool, Bolton v Hull ngoma ngumu!!!
Kigoli cha dakika za majeruhi, dakika ya 93, lilolifumaniwa na Fernando Torres limewapa ushindi Liverpool wa bao 1-0 huko Villa Park dhidi ya Wenyeji Aston Villa ambao hiki ni kipigo chao cha pili mfululizo kwenye Ligi Kuu baada ya kudundwa 3-0 na Arsenal mechi iliyopita.
Kwa ushindi huo, Liverpool sasa imeipiku Birmingham na kuchukua nafasi ya 7 kwenye msimamo wa Ligi.
Katika mechi nyingine ya Ligi Kuu iliyochezwa jana, Bolton na Hull City zilitoka sare 2-2.
Hull City walikuwa nyuma 2-0 kwa mabao ya Ivan Klasnic dakika ya 20 na dakika ya 61 Kevin Davies alifunga kwa kichwa bao la pili lakini mabao mawili ya Stephen Hunt yaliiwezesha Hull kupata droo.
MECHI ZA LIGI LEO: Jumatano, 30 Desemba 2009
[saa za bongo]
[saa 4 dak 45 usiku]
Portsmouth v Arsenal
[saa 5 usiku]
Man U v Wigan

No comments:

Powered By Blogger