Thursday 31 December 2009

Man United 5 Wigan 0
Manchester United, wakiwa nyumbani Old Trafford, wameibamiza Wigan mabao 5-0 katika mechi ya Ligi Kuu England na kujichimbia nafasi ya pili kwenye Ligi hiyo wakiwa na pointi 43 kwa mechi 20 huku vinara Chelsea wakiwa na pointi 45 kwa mechi 20.
Katika mechi ya mzunguko wa kwanza wa Ligi, Man U waliibamiza Wigan 5-0 Uwanja wa DW, nyumbani kwa Wigan, na mabao yote kwenye mechi hiyo yalifungwa kipindi cha pili.
Lakini katika mechi ya leo, hadi mapumziko Man U walikuwa mbele kwa mabao 3-0 Wafungaji wakiwa Wayne Rooney, dakika ya 28, Carrick, dakika ya 31 na Rafael dakika ya 44.
Kipindi cha pili Berbatov akapiga bao la 4 dakika ya 49 na Valencia akapachika la 5 dakika ya 74.
VIKOSI:
Man Utd: Kuszczak, Rafael Da Silva, Brown, Vidic, Evra, Valencia, Carrick, Fletcher, Park, Berbatov, Rooney.
AKIBA: Amos, Neville, Owen, Anderson, Welbeck, Fabio Da Silva, Obertan.
Wigan: Kirkland, Melchiot, Boyce, Bramble, Figueroa, Gomez, Thomas, Cho, Scharner, N'Zogbia, Rodallega.
AKIBA: Pollitt, Edman, Amaya, Scotland, Koumas, Sinclair, McCarthy.
REFA: Lee Mason

No comments:

Powered By Blogger