Tuesday 29 December 2009

LIGI KUU England: Chelsea kileleni!!!
• Goli la kujifunga wenyewe laipa ushindi Chelsea!!!
• Man City ushindi wa pili kwa Mancini!!!!
Kwenye mechi za jana za Ligi Kuu, Chelsea wakiwa ngomeni kwao Stamford Bridge walikuwa nyuma kwa bao 1-0 hadi mapumziko lakini kipindi cha pili wakapata mabao mawili moja likiwa la kujifunga wenyewe na kuilaza Timu ngumu Fulham 2-1.
Fulham walipata bao lao kupitia Gera dakika ya 4 na Drogba akaisawzishia Chelsea dakika ya 73.
Lakini dakika ya 75, Chris Smalling wa Fulham akajifunga mwenyewe na kuipa Chelsea ushindi wasiostahili.
Kwa ushindi huo, Chelsea wako mbele kwenye Ligi wakiwa na pointi 45 kwa mechi 20 wakifuatiwa na Manchester United, wanaocheza kesho na Wigan, wakiwa na pointi 40 kwa mechi 19. Timu ya 3 ni Arsenal, pia wanacheza kesho na ugenini na Portsmouth, na wana pointi 38 kwa mechi 18.
Nao Manchester City, wakicheza mechi yao ya pili chini ya Meneja mpya Roberto Mancini, wameshinda mechi yao ya pili baada ya kuikung’uta Wolves 3-0 ugenini.
Mabao ya Man City yalifungwa na Tevez, dakika ya 33 na 86, na Garrido dakika ya 69.
Tottenham Hotspurs, baada ya kuwafunga West Ham 2-0, sasa wameikwaa nafasi ya 4 kwenye Ligi wakiwa na pointi 37 kwa mechi 20.
MSIMAMO kileleni mwa LIGI KUU England: [Timu zimecheza mechi 20 isipokuwa inapotajwa]
1 Chelsea pointi 45
2 Man Utd pointi 40 [mechi 19]
3 Arsenal pointi 38 [mechi 18]
4 Tottenham pointi 37
5 Aston Villa pointi 35 [mechi 19]
6 Man City pointi 35 [mechi 19]
7 Birmingham pointi 32
8 Liverpool pointi 30 [mechi 19]
9 Fulham pointi 27 [mechi 19]
10 Sunderland pointi 23
MECHI ZA LIGI KUU LEO: Jumanne, 29 Desemba 2009
[saa 4 dak 45 usiku]
Aston Villa v Liverpool
[saa 5 usiku]
Bolton v Hull

No comments:

Powered By Blogger