Thursday 31 December 2009

KOMBE LA FA: Ni wikiendi ya FA, Ligi Kuu ni likizo!!!
Wikiendi hii ni mechi za Raundi ya Tatu ya Mitoano ya Kombe la FA tu na Timu za Ligi Kuu zimeingizwa rasmi na kupangiwa mechi kwenye Kombe hilo.
Timu nyingi za Ligi Kuu zinapambana na Timu za Madaraja ya chini lakini kuna baadhi ya mechi zinazozikutanisha Timu za Ligi Kuu zenyewe kama vile mechi ya Aston Villa v Blackburn, Wigan v Hull na West Ham v Arsenal.
Hivyo, wikiendi hii hamna mechi za Ligi Kuu ila Jumanne ijayo itakuwepo mechi moja ya Stoke v Fulham na Jumatano pia itakuwepo moja ya Arsenal v Bolton.
Wikiendi ya Januari 9 mechi za Ligi Kuu zitachezwa kama kawaida.
RATIBA: MECHI ZA FA CUP RAUNDI YA TATU
Jumamosi, 2 Januari 2010 [saa za bongo]
[saa 9 na nusu mchana]
Bristol City v Cardiff
[saa 12 jioni]
Accrington v Gillingham
Aston Villa v Blackburn
Blackpool v Ipswich
Bolton v Lincoln City
Brentford v Doncaster
Everton v Carlisle
Fulham v Swindon
Huddersfield v West Brom
Leicester v Swansea
MK Dons v Burnsley
Middlesbrough v Man City
Millwall v Derby
Nottingham Forest v Birmingham
Plymouth v Newcastle
Portsmouth v Coventry
Preston v Colchester
Scunthorpe v Barnsley
Sheffield Wednesday v Crystal Palace
Southampton v Luton
Stoke v York
Sunderland v Barrow
Torquay v Brighton
Tottenham v Peterborough
Wigan v Hull
[saa 2 na robo usiku]
Reading v Liverpool
Jumapili, 3 JanuarI 2010
[saa 10 jioni]
Man U v Leeds United
[saa 12 jioni]
Chelsea v Watford
Notts County v Forest Green
Sheffield United v QPR
[saa 1 na robo usiku]
West Ham v Arsenal
[saa 2 na robo usiku]
Tranmere v Wolves
Tembo kutua Bongo Jumamosi
Timu ya Taifa ya Cote D’ivoire, maarufu kama Tembo, watatua Dar es Salaam Jumamosi ili kupiga kambi ya mazoezi kwa matayarisho ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zitakazoanza kuchezwa huko Angola Januari 10.
Tembo watacheza na Timu ya Taifa ya Bongo, Taifa Stars, Uwanja wa Taifa Jumatatu usiku.
Kikosi hicho cha Ivory Coast kitawasili kikiwa na Watu 50.
Viingilio kwenye mechi hiyo ni kuanzia Shilingi 50,000/= hadi 5,000/=.
Tembo hao watakuwa na Mastaa wao kina Didier Drogba, Solomon Kalou, Yaya Toure, Aruna Dindane, Habib Kolo Toure na wengineo.
USHINDI WA 5-0 KWA WIGAN: Fergie aisifia Timu yake:
• Timu yote ilicheza murua!
• Rooney alikuwa kiboko!
Sir Alex Ferguson amesema alikuwa kwenye Xmas mbaya baada ya kufungwa mechi mbili dhidi ya Fulham 3-0 na Villa 1-0 lakini, baada ya kuikung’uta Wigan 5-0 hapo jana, yuko tayari kusherehekea bethdei yake akitimiza miaka 68 leo na pia mkesha wa Mwaka mpya.
Meneja huyo wa Manchester United anaamini Timu yake iko kwenye nafasi nzuri kuiandama Chelsea inayoongoza Ligi kwa vile tu wako pointi mbili nyuma yao.
Ferguson akizungumzia mechi ya jana alisema: “Wachezaji walijua ni lazima kufunga magoli kwani mwishoni mwa Ligi nani anajua pengine tofauti ya magoli itakuwa muhimu!”
Kero kubwa kwa Wigan hapo jana ilikuwa ni Winga wa Man U Antonio Valencia ambae Man U walimnunua kutoka Wigan mwanzoni mwa Msimu huu kwa Pauni Milioni 16. Valencia alifunga bao moja na kutengeneza matatu hapo jana.
Ferguson amesema: “Kwetu, muhimu ni kuwa Valencia alifunga goli moja na hilo ni goli lake la 6. Atafunga mengine zaidi msimu huu!!”
Kuhusu Rooney, ambae alifunga bao lake la 14 katika mechi 19 za Ligi, Ferguson amemsifu na kumwita ni kiboko.
Akizungumzia mechi ijayo ya Jumapili watakapocheza na Leeds United kwenye Kombe la FA, Ferguson amesema Kikosi tofauti kitacheza kikiwa na Chipukizi huku akidokeza Nahodha wake Gary Neville yuko fiti, Jonny Evans sasa yuko mazoezini na Ro Ferdinand tayari ameanza mazoezi.

No comments:

Powered By Blogger