Tuesday 29 December 2009

Van der Sar kapewa likizo, Nani kuuzwa?
Edwin van der Sar amepewa likizo ya dharura na Manchester United baada ya mkewe kuugua ghafla huko kwao Uholanzi na inasemekana hali yake si nzuri.
Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson amemruhusu Van der Sar kumuuguza mkewe hadi hali yake itakapotengamaa.
Van der Sar hajaichezea Man U tangu November 21 walipoifunga Everton 3-0 kwenye Ligi Kuu alipoumia goti.
Inategemewa Makipa Tomasz Kuszczak au Ben Foster ndio watakaokaa golini kwenye mechi ya kesho ya Ligi Kuu na Wigan huko Old Trafford.
Lakini katika siku za hivi kribuni Tomasz Kuszczak ndio amekuwa akidaka kila mechi.
Wakati huohuo, kuna uvumi mkubwa kuwa huenda Winga wa Man U Nani akatimkia Spain au Italy mwezi Januari dirisha la uhamisho likifunguliwa na inasemekana pia huenda akarudi kwao Ureno na kuchezea Benfica ili Man U wamchukue Nyota Chipukizi toka Argentina Angel di Maria toka Klabu hiyo.
Wakala wa Nani, Jorge Mendez, amedokeza kuwa yupo mbioni kushughulikia suala la Nani.
Kuwafunga “Vibonde” wawili, Mancini aota Ubingwa Man City!!
Roberto Mancini, Meneja mpya wa Manchester City, ambaye alianza himaya yake kwa kuwafunga ‘Vibonde’ Stoke City 2-0 Desemba 26 na kisha jana kuibwaga Wolves 3-0, ameanza majigambo na kudai Timu yake ni nzuri sana kuliko alivyofikiria mwanzo na wana uwezo wa kutwaa Ubingwa wa England.
Awali, alipoingia tu Man City wiki moja iliyopita, Mancini alitangaza lengo lake ni kumaliza miongoni mwa Timu Bora nne Msimu huu na kisha kutwaa Ubingwa Msimu ujao.
Mancini ametamba: “Tumebakiza mechi 19 za Ligi na uwezo tunao wa kuwa Mabingwa! Tuna Timu nzuri!”
Mancini aliongeza kwa kusema wiki yake ya kwanza hapo Man City imekuwa nzuri ingawa ana listi ya majeruhi kibao wakiwemo Wachezaji kina Stephen Ireland, Roque Santa Cruz, Joleon Lescott, Wayne Bridge, Shaun Wright-Phillips na Nedum Onuoha.
Vilevile, atawakosa Kolo Toure na Emmanuel Adebayor kwa mwezi Januari watakaposafiri kwenda kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika huko Angola.

No comments:

Powered By Blogger