Sunday 27 December 2009

Mitutu ikiongozwa na Fabregas yaiua Villa!!
Katika mechi ya Ligi Kuu leo Arsenal wakiwa nyumbani Uwanjani Emirates wameipiga Aston Villa mabao 3-0 na mabao mawili ya kwanza yakifungwa na Nahodha wao Cesc Fabregas alieanza mechi hii akiwa benchi na kuingizwa mara baada ya Kipindi cha Pili kuanza.
Fabregas alifunga bao la kwanza kwa frikiki murua kwenye dakika ya 65 na kuongeza bao la pili baada ya pasi tamu ya Theo Walcott dakika ya 80.
Abou Diaby akaongeza bao la 3 dakika ya 90.
Kwa ushindi huo, Arsenal sasa wako nafasi ya pili na wamecheza mechi 18 na wana pointi 38 na wako nyuma ya Chelsea wanaoongoza kwa kuwa na pointi 42 kwa mechi 19.
Mabingwa Watetezi Manchester United, wanaocheza na Hull City muda si mrefu kuanzia sasa, wako nafasi ya 3 wakiwa wamecheza mechi 18 na wana pointi 37.
Aston Villa wako nafasi ya 4, wamecheza mechi 19 na wana pointi 35.
VIKOSI:
Arsenal: Almunia, Sagna, Gallas, Vermaelen, Traore, Song Billong, Denilson, Nasri, Diaby, Eduardo, Arshavin.
AKIBA: Fabianski, Fabregas, Vela, Walcott, Ramsey, Silvestre, Eboue.
Aston Villa: Friedel, Luke Young, Dunne, Cuellar, Warnock, Ashley Young, Petrov, Milner, Downing, Agbonlahor, Heskey.
AKIBA: Guzan, Sidwell, Carew, Delph, Reo-Coker, Beye, Collins.

No comments:

Powered By Blogger