Tuesday 29 December 2009

LEO NI:
• Aston Villa v Liverpool
• Bolton v Hull City
Leo usiku kutakuwa na mechi mbili za Ligi Kuu England kati ya Aston Villa v Liverpool na nyingine ni Bolton v Hull.
Kwa Mashabiki wengi mechi yenye mvuto zaidi ni ile kati ya Villa v Liverpool itakayochezwa Villa Park kwa sababu tu Villa Msimu huu imechachamaa kuwania kumaliza Ligi ikiwa kwenye Timu Bora nne ili wafuzu kucheza Ulaya kwenye UEFA CHAMPIONS LEAGUE Msimu ujao na Liverpool awali iliota kutwaa Ubingwa Msimu huu lakini baada ya mwendo mbovu, ikiwemo kufungwa mechi 7 za Ligi na sare nyingi, sasa wako nafasi ya 8 kwenye Ligi na, bila shaka, wanaombea tu kumaliza wakiwa kwenye Timu Bora nne.
Villa katika mechi yake ya mwisho ilitandikwa mabao 3-0 na Arsenal Uwanjani Emirates na leo itashuka kwao ikitaka kufuta matokeo hayo mabaya.
Liverpool walishinda mechi yao ya mwisho kwa bao 2-0 dhidi ya Wolves walipokuwa nyumbani Anfield.
Katika mechi ya leo, Villa watamkosa Winga wao machachari Ashley Young ambae ana adhabu ya kufungiwa mechi moja baada ya kupata jumla ya Kadi 5 za Njano.
Liverpool watamkosa Kiungo wao mahiri kutoka Argentina Javier Mascherano ambae ana adhabu ya kufungiwa mechi.
Refa katika mechi hiyo ni Peter Walton.

No comments:

Powered By Blogger