Sunday 27 December 2009

Fabregas aipa ushindi Arsenal lakini...........!!!!!!!
Nahodha wa Arsenal Cesc Fabregas ambae leo ndie alieipa ushindi Timu yake baada ya kuingizwa Kipindi cha Pili na kufunga bao 2 zilizoipa ushindi Arsenal wa bao 3-0 dhidi ya Aston Villa kwenye Ligi Kuu Uwanjani Emirates alilazimika kutolewa huku zikiwa zimebaki dakika 6 mpira kumalizika baada ya kujitonesha sehemu aliyoumia hivi karibuni na ambayo ndio iliyomfanya asianze mechi hii tangu mwanzo.
Taarifa zinasema kuna hatari Fabregas akawa nje ya uwanja kwa mwezi mmoja baada ya kujiumiza tena musuli ule ule wa mguu uliomfanya akose mechi hivi karibuni.
Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, amethibitisha habari za kuumia Nahodha wake ingawa amesema bado hawajajua atakuwa nje kwa muda gani. 
Wenger vilivile alidokeza kuwa mwezi Januari wanaweza kuingia sokoni dirisha la uhamisho litakapofunguka kununua Mshambuliaji mmoja ili kuziba pengo la Robin van Persie ambae atakuwa nje mpaka Aprili au Mei kuuguza enka yake.

No comments:

Powered By Blogger